• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

Waandishi wa Habari wapata mafunzo ya usalama mahala pa kazi

Posted on: September 19th, 2018

Waandishi wa Habari kutoka mikoa saba ya Kanda ya Ziwa, wamepatiwa mafunzo ya namna wanavyoweza kutumia mbinu mbalimbali kuhakikisha usalama wao wanapokuwa wakitekeleza majukumu yao.

Akitoa taarifa  wakati wa ufunguzi wa mafunzo hayo Kaimu Katibu Mtendaji wa Tume ya Taifa  (UNESCO) Tanzania Dr. Moshi Kimizi alisema, lengo la mafunzo hayo ni kuwajengea uwezo waandishi wa habari husasani wa vijijini kuhusu njia bora za kufanya kazi zao kwa ufanisi,  usalama na kuimarisha uhuru wa vyombo vya habari nchini .


"Katika nchi mbalimbali duniani waandishi wanafanya kazi katika mazingira magumu na hatarishi,  takwimu zinaonyesha kwamba, duniani mwandishi mmoja anauwawa kila baada ya siku tano katika harakati za kutekeleza majukumu yake ya kiuandishi ambapo katika nchi za Afrika Kusini mwa Jangwa la Sahara waandishi 73 walipoteza maisha kwa kipindi cha miaka miwili iliyopita,"alisema Kimizi.


Aliongeza kuwa, katika baadhi ya nchi duniani, mamia ya waandishi wa habari wanauawa, wanatekwa, wanatishwa, wananyamazishwa, wanadhalilishwa na kuwekwa chini ya ulinzi bila kufuata sheria kwa sababu ya kusema ukweli kwa kueleza maovu mbalimbali yanayoidhuru jamii husika, ndiyo chachu iliyowafanya  UNESCO kuandaa mafunzo hayo.

"Mtajifunza na kujadili mada mbalimbali zinazolenga kuimarisha uandishi wenu katika mtazamo wa usalama ambapo, baadhi ya mada nyeti zikiwa ni kujifunza sheria za uandishi wa habari, maadili ya uandishi wa habari, sheria za habari za kimataifa ambazo Tanzania inazitambua, sera za vyombo vya habari, bima kwa waandishi wa habari na namna nyingine za kuhakikisha usalama wao pamoja na mikataba ya ajira, hivyo baada ya mafunzo hayo kila mmoja  atayatafasiri kwa vitendo ili kuepukana na habari zinazoweza kuwaletea madhara," aliongeza.

Kwa upande wake Kaimu Katibu Tawala Mkoa wa Mwanza Mhandisi Warioba Sanya ambaye alizungumza kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. John Mongella alisema, suala la usalama na ulinzi kwa waandishi ni lenye umuhimu  hasa ukizingatia majukumu mahasusi waliyonayo ya kuahabarisha ,kuuelimisha na kuushawishi umma  kuhusu masuala mbalimbali yanayohusu maendeleo na ustawi wa jamii.

Alisema, pamoja na umuhimu huo wa waandishi, takwimu na taarifa za mashirika mbalimbali husasani UNESCO zinaonyesha kuwa takriban waandishi 820 wanauawa katika kipindi cha miaka 10 iliyopita wakati wakitimiza majukumu yao ,ili kufahamu njia bora zinazopatikana kwa urahisi Serikali kwa kushirikiana na tume hiyo imechukua uamuzi  mahsusi wa kufanya uwezeshaji na  kuendesha mafunzo hayo.

" Nimetaarifiwa mafunzo hayo yatafanyika hapa Mwanza na huko Dodoma yakishirikisha waandishi kutoka takriban mikoa yote ya Tanzania ambapo kwa hapa wametoka Mwanza, Shinyanga, Tabora, Geita, Mara, kagera na Simiyu hivyo matumaini yangu kwa kupitia  mafunzo haya tunaweza kuona mabadiliko makubwa katika sekta ya uandishi wa habari husasani usalama na ulinzi wakiwa kazini," alisema Sanya.

Kwa upande wake mmoja wa wakufumzi wa mafunzo hayo kutoka chuo kikuu cha Dar es salaam kupitia shule kuu ya Uandishi wa Habari na Mawasiliano kwa Umma (SJMC)  Dotto Kuhenga alisema, mara nyingi waandishi wa habari wanasahau ulinzi na usalama wao wakati wa majukumu yao hivyo ni wakati kutambua na kuzielewa njia za kujilinda dhidi ya hatari yoyote inapojitokeza ili kupunguza ongezeko la waandishi kupoteza maisha.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • SERIKALI KUIMARISHA USHIRIKIANO NA SEKTA BINAFSI MWANZA

    May 10, 2025
  • SERIKALI KUNUNUA MTAMBO RASMI WA KUSAFISHA ZIWA VICTORIA

    May 10, 2025
  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.