• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

Wamiliki vyombo vya majini wazingatie upakiaji abiria,upangaji mizigo

Posted on: August 1st, 2019


Wamiliki wa Vyombo vya usafiri wa majini wametakiwa kuzingitia uwezo wa vyombo vyao badala ya kuendekeza tabia ya kuhesabu abiria wanaoingia kwenye chombo na kuhatarisha usalama wao na chombo.

Rai hiyo imetolewa  jijini Mwanza na Meneja Usajili, Ukaguzi na Udhibiti wa Vyombo vya Majini wa Shirika la Uwakala wa Meli Tanzania (TASAC), Mhandisi Alfred Waryana, baada ya kutembelea kivuko cha Kamanga Ferry.


Alisema wamiliki wa vyombo vya usafiri wa majini pamoja na wafanyakazi wao, wazingatie utaratibu wa kupakia abiria na mizigo ili kulinda usalama wa watumia huduma na kuepusha madhara na ajali za majini.


Mhandisi Waryana ambaye ameongozana na wajumbe wa Bodi ya Wakurugenzi wa TASAC na Menejimenti ya shirika hilo, amewaagiza manahodha kuwaelimisha abiria kuhusu matumizi ya vifaa vya kuokolea maisha kabla ya chombo kuondoka gatini na kuwataka wamiliki kuajiri manahodha na mabahari wenye viwango vinavyotambulika.

“Nitoe rai kwa wamiliki na wafanyakazi kuacha tabia ya kuhesabu abiria wanapoingia kwenye chombo badala ya kuzingatia uwezo wa chombo ili kulinda usalama.Pia wazingatie utaratibu wa kupakia na kupanga aina ya mizigo na ipangwe kabla ya abiria kuingia ndani ya chombo,”alisema Mhandisi Waryana.

Alieleza kuwa manahodha wa vyombo wahakikishe wanasimamia upangaji wa mizigo yote kwenye vyombo na kuonya kuwa watafanya makosa endapo wataacha jukumu hilo kusimamiwa na watu wasio na utaalamu jambo linaloweza kusababisha ajali kutokana na upangaji mbaya wa mizigo.

Aidha,alisistiza kuwa chombo kinapofika ng’ambo ya pili sharti abiria washuke kwanza kabla ya magari ili kuzuia mwingiliano na kwamba vyombo vya majini  kabla ya kuanza kutoa huduma vinatakiwa kukaguliwa,kusajiliwa na kupewa vyeti na hivyo  wamiliki wazingatie masuala hayo kwa kuwa ni ya msingi.

Meneja udhibiti na usajili huyo aliongeza kuwa ukaguzi unaofanyika huainisha  vifaa vyote vinavyotakiwa kwenye chombo, sifa za manahodha na mabaharia na mfumo wa upakiaji abiria na mizigo.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.