• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

Misungwi yapiga vita Ukatili,Unyanyasaji kijinsia

Posted on: July 10th, 2018


Mkuu wa Wilaya ya Misungwi, Mhe.Juma Sweda ameyataka makundi yote ya kijamii Wilayani humo kushirikiana kupiga vita ukatili na unyanyasaji wa kijinsia ambao ni miongoni mwa vikwazo dhidi ya juhudi za Serikali za kupambana na umaskini nchini.

Akizungumza wakati wa hafla ya uzinduzi wa kampeni ya wiki nane ya kutokomeza ukatili kwa wanawake na wasichana inayoendeshwa na Shirika lisilo la Kiserikali la Kivulini la jijini Mwanza kwa kushirikiana na Halmashauri ya Wilaya hiyo, amesema pesa wanazopata wanaume wa Wilayani humo kutokana na mavuno zinawalevya, matokeo yake ndoa zinavunjika, watoto wanashindwa kusoma na hali ya maisha inakuwa ngumu kwenye familia.

“Kaa na familia yako kipindi hiki cha mavuno mpange kitu gani cha maendeleo mnafanya, kwa ajili ya maendeleo yenu lakini pia kusomesha watoto wenu kwa kuwatimizia mahitaji na vifaa vya shukeni ili wawe nadhifu,”alisema Sweda.


Mkurugenzi Mtendaji wa Wilaya hiyo Eliud Mwaiteleke alisema, kampeni hiyo itahusisha Kata 27, Vijiji 113 na Vitongoji 724,ambapo walikubaliana kila kata ifanye uzinduzi kuweka msukumo kwa jamii wa kupinga ukatili kwa wanawake na wasichana na kukuza hali ya kujiletea maendeleo kwenye Kaya, kusomesha watoto na kupambana na mimba za utotoni.

Naye Mkurugenzi wa Shirika la Kimvulini Yassin Ally alisema, ni wakati sasa wa jamii kubadilika na kuondokana na imani potofu kwa kuzani kila maumivu ni kurogwa sambamba na kufuja pesa zitokanazo na mavuno kwa kutumia na wanawake wa nje badala ya kufanya maendeleo kwa kujenga nyumba nzuri na kusomesha watoto.

“Unalalia godoro Dodoma Ngumaru (godoro lililotengenezwa kwa majani yaliyokauka) ukiamka asubuhi shingo inakuuma, mgongo unauma halafu unasema nani kanikalia usiku unakimbilia kwa waganga wa kienyeji kwanini usinunue godoro zuri? Tubadilikeni ndugu zangu”alisema Ally.

Hata hivyo Wanawake na wanaume Wilayani humo walitumia kampeni hiyo kusukumiana lawama kila upande ukiushutumu mwingine kusababisha vitendo hivyo vikiwemo mahusiano ya kimapenzi nje ya ndoa.

Fransico Kiyumbi alikuwa wa kwanza kuanza kurusha madongo dhidi ya wanawake akisema baadhi yao huwafanyia waume zao ukatili na unyanyasaji kijinsia kwa kuwanyima chakula na unyumba kutokana na kuwa na mahusiano ya kimapenzi nje ya ndoa.

Regina Kubunga alijibu mapigo kwa kutaja madhaifu ya wanaume ikiwemo baadhi yao kutotimiza wajibu wa kuhudumia familia kiasi cha wanawake kulazimika kutumia akili na mbinu mbadala kutafuta fedha za kugharamia chakula na mahitaji mengine ya familia ikiwemo elimu ya watoto.

Matangazo

  • WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA KIDATO CHA KWANZA MKOA WA MWANZA MWAKA 2021 December 18, 2020
  • Matokeo ya Uchaguzi wa Wanafunzi Waliochaguliwa Kujiunga na Kidato cha Kwanza 2018 Shule za Sekondari za Serikali Mkoa wa Mwanza December 13, 2017
  • Ziara ya Mhe. Mkuu wa Mkoa kwa ajili ya kufanya ufuatiliaji katika shule za Msingi na Sekondari Mkoa wa Mwanza 2018 January 10, 2018
  • Ufunguzi wa Mashindano ya UMISSETA na UMITASHUMTA Kitaifa Mkoa wa Mwanza. June 07, 2018
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • AGA KHAN Yatoa Vifaa vya Bilioni 1.5 Kuepusha vifo vya mama na mtoto Mwanza

    December 22, 2020
  • Kikao cha bodi ya Barbara chapanga mikakati ya mafanikio Mwanza

    December 21, 2020
  • Mwanza Kwanza Toleo la pili kwa habari mbalimbali Mkoa wa Mwanza

    December 12, 2020
  • Elimu ya maadili yatolewa Mwanza kwa Viongozi

    December 10, 2020
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe.John Mongella akifungua Baraza la biashara katika kikao kilichofanyika kwenye ukumbi wa mkikutano uliopo katika ofisi ya Mkoa uliojumuisha wajumbe mbalimbali wa Baraza hilo wa Mkoa wa Mwanza.
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Regional Drive Mkabala na Ofisi za TRA

    S.L.P: S.L.P. 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras.mwanza@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.