• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

WAZEE ZINGATIENI LISHE BORA KUJIKINGA NA MARADHI - RC MTANDA

Posted on: September 29th, 2025

Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Said Mtanda ametoa rai kwa wazee kula vyakula vyenye lishe bora kwa kufuata mlo kamili na kuzingatia makundi yote muhimu ili kujihakikishia afya imara na kuepuka maradhi hususani yasiyoambukiza.

“Wazee tuache tabia ya kula vyakula bila kufuata mlo kamili kwa mfano mtu asubuhi anakula wali, mchana anakula wali na usiku pia anakula wali wakati huo ni wanga ambao kazi yake ni kuleta nguvu na kubadilika kuwa sukari na mafuta hivyo ni vyakula ambavyo havitusaidii kwa afya yetu.” Mhe. Mtanda.

Mhe. Mkuu wa Mkoa ametoa rai hiyo leo tarehe 29 Septemba, 2025 wakati akihutubia katika kongamano la Siku ya Wazee duniani lililoadhimishwa kimkoa katika ukumbi wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa kwa kuwakutanisha wazee zaidi ya 200 waliojadili kuhusu mustakabali wa maisha yao.

Aidha, amewahakikishia wazee hao kuwa serikali itaendelea kuboresha maisha yao katika nyanja mbalimbali kama kuwapatia huduma bora za afya bila malipo ambapo akabainisha jumla ya wazee Elfu 97 wametambuliwa na kupewa vitambulisho mkoani humo.

Kadhalika, amewasihi kundi linaloelekea kwenye uzee kuwekeza katika shughuli za uzalishaji mali kama kilimo, uvuvi na ufugaji ili kujiwekea akiba ya uchumi imara wakati wa uzee jambo litakalowasaidia kuondokana na msongo wa mawazo.

Mganga Mkuu wa Mkoa huo Dkt. Jesca Lebba amesema Mwanza yenye vituo 569 vya kutolea huduma unatoa kipaumbele kwa kundi hilo na kwamba jumla ya wazee elfu 78 wamehudumiwa 2024/25 na kupitia mabaraza ya wazee halmashauri zinawawezeshwa kwa kuwahusisha na shughuli mbalimbali za uchumi.

Akiongea kwa niaba ya mwenyekiti, Mzee Juma Ngeleja ametumia wasaa huo kuishukuru serikali kwa kuendelea kuboresha huduma za kijamii kama kujengwa kwa zahamati vijijini na uwepo wa madawati maalumu ya kuwahudumia kwa kipaumbele kwani ni ishara kuwa serikali inajali afya ya wazee.

Oktoba Mosi ya kila mwaka ni siku ya wazee duniani ambapo kitaifa hapa nchini siku hiyo itaadhimishwa kesho kutwa mkoani Ruvuma chini ya Kaulimbiu isemayo ‘Wazee tushiriki uchaguzi Mkuu 2025 kwa ustawi wa jamii yetu’.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • WAZEE ZINGATIENI LISHE BORA KUJIKINGA NA MARADHI - RC MTANDA

    September 29, 2025
  • WANANCHI WAASWA KUBADILI MTINDO WA MAISHA ILI KULINDA AFYA YA MOYO

    September 29, 2025
  • PROGRAMU YA WANAWAKE NA SAMIA SI YA KUBEZWA NI FURSA YA KUKUA KIUCHUMI - RC MTANDA

    September 27, 2025
  • RAS BALANDYA APOKEA UGENI KUTOKA WIZARA YA MADINI

    September 26, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.