• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

E-MABORESHO IMEKUJA KIMKAKATI KUMALIZA RUSHWA NCHINI- RAS BALANDYA

Posted on: October 9th, 2025

Katibu Tawala Mkoa wa Mwanza Bw. Balandya Elikana amewataka wajumbe wa Kamati za Utekelezaji wa mkakati wa kitaifa wa Kuzuia na kupambana na Rushwa kutumia mfumo wa E-Maboresho kwa ufanisi ili kusaidia kumaliza tatizo la Rushwa nchini.

Ametoa rai hiyo leo tarehe 09 Oktoba, 2025 wakati akifungua mafunzo ya mfumo wa kielektroniki wa utekelezaji wa mkakati wa IV wa kitaifa wa kuzuia na kupambana na Rushwa yaani E-Maboresho katika ukumbi wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa.

Amesema, serikali inatamani kuona rushwa imetokomezwa kabisa nchini ili kuhakikisha taifa linasonga mbele kwa mujibu wa katiba ya nchi, hivyo matumizi ya mfumo huo yatawaimarisha wajumbe wa kamati kuweza kuchakata taarifa na kuwasilisha kwa wakati kwa ajili ya hatua zinazofuata.

Aidha, Bw. Balandya amemithilisha uboreshwaji mkubwa wa miradi ya maendeleo katika sekta za miundombinu, Elimu, Maji, Afya, Kilimo, Uchukuzi na Miundombinu na mafanikio ya mikakati ya kupambana na rushwa kwani imeleta matumizi mazuri ya fedha kwenye miradi.

Mratibu wa Mafunzo hayo kutoka OR Ikulu Bi. Christina Maganga amebainisha kuwa mafunzo hayo ya matumizi ya mfumo wa kielektroniki wa utekelezaji wa mkakati wa kitaifa wa kuzuia Rushwa E-Maboresho yamelenga kuwajengea uwezo Wenyeviti na Makatibu wa Kamati hizo pamoja na Maafisa TEHAMA.

Aidha, amefafanua kuwa mafunzo hayo yalikwishafanyika katika mikoa 17 ukiwemo Mkoa wa Mwanza na kwamba kwa siku mbili hizo yamewakutanisha wajumbe kutoka mikoa ya Mara, Simiyu na Kagera ambao watajengewa uwezo juu ya utumaji wa taarifa za utekelezaji wa kila robo kuhusu masuala ya mkakati wa Taifa dhidi ya rushwa ili maamuzi yatolewe kwa wakati.


Wakati akijinasibu na uwepo wa vivutio lukuki vya utalii mkoani humo na kuwahamasisha kuvitembelea wawapo kwenye mafunzo hayo, Katibu Tawala amewasihi wajumbe wa mafunzo hayo kuhakikisha wanapiga kura katika uchaguzi mkuu wa Oktoba 29, 2025

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • TUME YA MIPANGO YAENDELEA KUTOA MAFUNZO YA DIRA YA TAIFA YA MAENDELEO 2050 KWA TAASISI BINAFSI

    October 09, 2025
  • E-MABORESHO IMEKUJA KIMKAKATI KUMALIZA RUSHWA NCHINI- RAS BALANDYA

    October 09, 2025
  • WAZEE ZINGATIENI LISHE BORA KUJIKINGA NA MARADHI - RC MTANDA

    September 29, 2025
  • WANANCHI WAASWA KUBADILI MTINDO WA MAISHA ILI KULINDA AFYA YA MOYO

    September 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.