• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

Mwanza Kutokomeza vifo vya mama,watoto wachanga

Posted on: April 3rd, 2019

Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Mhe. John Mongella amewasainisha  kiapo  cha uwajibikaji wakuu wa wilaya zote za Mkoa huo  juu ya kupunguza vifo vya wajawazito na watoto wachanga ambapo amewataka kila mmoja awajibike katika eneo lake na  kutoa taarifa ya za utekelezaji.

Mhe.Mongella alisema kutokana na jitihada za Serikali za kupunguza vifo vya mama na watoto wachanga, mwaka 2018 vifo hivyo vimepungua na kufikia 151 lakini kuanzia Januari mwaka huu tayari vifo 46 vitokanavyo na uzazi vimetokea ndani ya mkoa huo.

“Sababu zinazoelezwa kusababisha vifo hivyo ni kwamba shinikizo la damu, kifafa cha mimba, kuvuja damu nyingi lakini sababu zingine inadaiwa zinatokana na maamuzi katika familia husika, vile vile na sisi viongozi wa umma tunahusika katika maeneo fulani.

“Sasa mimi    kama Mkuu wa Mkoa naamua niingia mikataba na wakuu wa wilaya zote za mkoa huu, mkataba huu pia utawahusu wakurugenzi,meya na wenyeviti wa halmashauri, viongozi hawa  niliowataja itakuwa rahisi mimi kuwabana na ndio maana nataka waje hapa mbele waweke sahihi zao.

“Kila mmoja akitoka hapa aende awajibike katika eneo lake kwa kufuatilia maendeleo ya utoaji huduma katika vituo, zahanati na hospitali zao, pia ni muhimu wakashuke  ngazi za chini kuanzia vitongoji hadi vijiji na kuwatambua wajawazito na  maendeleo yao, ikitokea kifo  katika eneo lako unapaswa kutoa  sababu za msingi kilichosababisha,”alisema Mongella.


Mongella alisema kumekuwapo na tabia ya viongozi  wengi wa Serikali kuzungumza wakiwa maofisini  kitendo ambacho kimeshindwa kuwa na mafanikio chanja kwa jamii  juu ya mikakati inayopangwa, hivyo ni wakati muafaka kwenda vijijini na kuzungumza moja kwa moja na wananchi.


Alisema licha ya Serikali kuboresha sekta ya afya kwa kujenga vituo vya afya, zahanati, hospitali sambamba na kuongeza bajeti lakini tunapaswa kujitafakari kinachosababisha vifo vya mama na watoto vinaendeleo kutokea, hivyo aliwataka wadau wote wa afya, vyombo vya habari, viongozi wa dini na waganga wa tiba asili kuungana na kuelimisha jamii kuwahi kwenye tiba sahihi.

Naye Mratibu wa Afya mama na mtoto Mkoa wa Mwanza, Cecilia Mrema  kuna haja ya Serikali kuboresha magari ya kubebea wagonjwa mkoani humo kwani kati ya ambulesi 9 kati 25 zilizopo ndizo zilizo na vifaa vyote vya kutolea huduma wakati mgonjwa akipelekwa hospitali ya rufaa.


Alisema katika Mkoa wa Mwanza sababu nyingi za vifo hivyo ni  upungufu wa damu, vifaa, baadhi ya watumishi wa sekta ya afya kutokuwa na uelewa zaidi kwa wagonjwa wanaohitaji msaada wa haraka, gari za wagonjwa kutokuwa na mafuta na vifaa vyote vya tiba.

Vile vile alisema wajawazito kutumia dawa za kienyeji, kifafa cha mimba ambapo aliwataka akinamama kuhudhuria katika vituo vya afya  ili kupata tiba sahihi.

Kwa upande wa Mganga Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Dkt. Thomas Rutachunzibwa alisema  uzinduzi wa kampeni ya uwajibikaji katika kuzuia vifo vitokanavyo na uzazi yenye kauli mbiu ya ‘Jiongeze Tuwavushe salama’  ni utekelezaji wa agizo la Makamu wa Rais, Samia Hassan Suluhu alilolitoa Novemba mwaka jana kwa kuelekeza kila mkoa kuweka mikakati ya kupunguza vifo vya mama na mtoto.

Alisema   kutokana na agizo hilo, mkoa wa Mwanza  umejipanga kupitia kampeni hiyo kupunguza idadi ya vifo vya mama na mtoto ambapo aliwataka watoa huduma kuongeza kasi kwani Serikali imeelekeza nguvu kubwa katika sekta ya afya.

Matangazo

  • WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA KIDATO CHA KWANZA MKOA WA MWANZA MWAKA 2021 December 18, 2020
  • Matokeo ya Uchaguzi wa Wanafunzi Waliochaguliwa Kujiunga na Kidato cha Kwanza 2018 Shule za Sekondari za Serikali Mkoa wa Mwanza December 13, 2017
  • Ziara ya Mhe. Mkuu wa Mkoa kwa ajili ya kufanya ufuatiliaji katika shule za Msingi na Sekondari Mkoa wa Mwanza 2018 January 10, 2018
  • Ufunguzi wa Mashindano ya UMISSETA na UMITASHUMTA Kitaifa Mkoa wa Mwanza. June 07, 2018
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • AGA KHAN Yatoa Vifaa vya Bilioni 1.5 Kuepusha vifo vya mama na mtoto Mwanza

    December 22, 2020
  • Kikao cha bodi ya Barbara chapanga mikakati ya mafanikio Mwanza

    December 21, 2020
  • Mwanza Kwanza Toleo la pili kwa habari mbalimbali Mkoa wa Mwanza

    December 12, 2020
  • Elimu ya maadili yatolewa Mwanza kwa Viongozi

    December 10, 2020
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe.John Mongella akifungua Baraza la biashara katika kikao kilichofanyika kwenye ukumbi wa mkikutano uliopo katika ofisi ya Mkoa uliojumuisha wajumbe mbalimbali wa Baraza hilo wa Mkoa wa Mwanza.
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Regional Drive Mkabala na Ofisi za TRA

    S.L.P: S.L.P. 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras.mwanza@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.