• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

Posted on: May 2nd, 2025

DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.


Serikali imetangaza kuwa daraja la JPM Kigongo-Busisi, linalounganisha wilaya za Sengerema na Misungwi mkoani Mwanza lipo tayari kuanza kutumika muda wowote kuanzia sasa baada ya kukamilika kwa zaidi ya asilimia 99 ya ujenzi wake.

Taarifa hiyo imetolewa na Msemaji Mkuu wa Serikali ambaye pia ni Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Bw. Gerson Msigwa wakati wa ziara yake ya kukagua utekelezaji wa miradi ya kimkakati mkoani Mwanza ikiwemo ya vivuko na daraja hilo muhimu.

Msigwa amesema kukamilika kwa daraja hilo ni hatua kubwa ya maendeleo kwani linakwenda kumaliza changamoto ya usafiri kwa wananchi wa mikoa ya Kanda ya ziwa na hata wale wanaotoka nje ya nchi wanaovuka ziwa Victoria kuingia au kutoka mkoani Mwanza.

“Daraja hili linatarajiwa kuanza kutumika ndani ya mwezi Mei.Hii ni neema kwa Watanzania, hususan wa mikoa ya kanda hii, kwani litaimarisha biashara, usafiri na fursa nyingine za kiuchumi,” amesema Msigwa.

Aidha, Msigwa amesema serikali inaendelea kutekeleza miradi mingine ya kuboresha usafiri wa majini kwa kujenga vivuko vipya katika maeneo mbalimbali ya Ziwa Victoria ili kurahisisha huduma kwa wananchi.

Katika hatua nyingine, Msigwa ametembelea pia ujenzi wa meli mpya ya MV Mwanza ambao umefikia asilimia 96. Alisema kazi zilizobaki ni kufunga viti na vitanda, na meli hiyo itaanza kutoa huduma kwa wananchi muda si mrefu.

Ameeleza kuwa miradi hii yote ni sehemu ya dhamira ya serikali ya Awamu ya Sita ya kuimarisha miundombinu ya usafiri na kuchochea maendeleo ya kiuchumi kwa wananchi wa Kanda ya Ziwa na Taifa kwa ujumla.

Katika ziara hiyo, Msigwa aliambatana na waandishi wa habari kutoka mikoa ya Mwanza na Shinyanga, waliopata fursa ya kujionea maendeleo ya utekelezaji wa miradi hiyo ya kimkakati.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • MWANZA, SIMIYU ZANG'ARA UTAMILIFU DARASA LA SABA KANDA YA ZIWA

    May 30, 2025
  • RAS MWANZA AZINDUA RASMI MRADI WA KUPAMBANA NA UGONJWA WA SELI MUNDU

    May 30, 2025
  • WAANDISHI WA HABARI MWANZA WAPIGWA MSASA MIKAKATI YA KUTOKOMEZA WATOTO WA MITAANI

    May 29, 2025
  • RAS MWANZA AWATAKA VIONGOZI WA UMMA KUDUMISHA NIDHAMU NA UFANISI KAZINI

    May 26, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.