• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

DC MKALIPA AVIPONGEZA VIKUNDI VYA JOGGING KWA KUANDAA TAMASHA LENYE HAMASA

Posted on: October 25th, 2025

Mkuu wa Wilaya ya Ilemela Mhe. Amir Mkalipa amevipongeza vikundi vya mbio za pole pole (Jogging) mkoani humo kwa kuandaa tamasha la kuwahamasisha wananchi kufanya mazoezi kwa ajili ya kulinda afya zao dhidi ya magonjwa yasiyoambukiza.

Amesema hayo akimuwakilisha Mkuu wa Mkoa Mwanza katikaTamasha la mbio za pole zenye lengo la kujenga afya na kupongeza maboresho katika sekta ya afya lililofanyika leo Oktoba 25, 2025 kwa kukimbia kuanzia viwanja vya Furahisha hadi hospitali ya Rufaa ya Mkoa Sekou-Toure, kuchangia damu pamoja na kufanya usafi katika hospitali hiyo.

Ameongeza kwa kuishukuru serikali ya awamu ya Sita kwa kuboresha sekta afya mkoani humo kwa kuongeza ajira na kupunguza uhaba wa watumishi, kuleta vifaa tiba, madawa pamoja na kuboresha huduma za kibingwa katika hospitali ya Mkoa ya rufaa Sekou-Toure na hospitali ya kanda Bugando.

“Zaidi ya watumishi 600 wameongezeka sekta ya Afya mkoani Mwanza huku huduma za matibabu ya saratani zikipatikana katika hospital ya kanda Bugando na dawa zikipatikana kutoka asilimia 75 na kufikia asilimia 97 kwa kipindi cha miaka minne iliyopita”. Amesema Mhe. Mkalipa.


Sambamba na hayo Mhe. Mkalipa amewataka wananchi Mkoani Mwanza kuendelea kuilinda amani ya Mkoa na nchi kwa ujumla huku wakijitokeza kushiriki katika zoezi la kupiga kura kwa amani na kuchagua viongozi ambao wataleta maendeleo yenye tija katika taifa na maeneo yao wanayoishi.

Naye Msimamizi wa kituo cha michezo Biro na muandaaji wa tamasha la mbio za pole Bw. Hamisi Bilali amesema lengo kuu la kuandaa tamasha hilo ni kupongeza maendeleo yaliyofanyika ndani ya serikali ya awamu ya Sita katika huduma za afya na kuwahimiza wananchi kutunza afya zao.

Kwa upande wake Mganga Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Dkt. Jesca Lebba amesema sekta ya afya imeendelea kua bora kwa kutoa huduma za matibabu ya dharura katika hospitali za Halmashauri zote, uboreshaji wa mashine za Xray, CT Scan na utra sound sambamba na hayo serikali imetoa fedha Bilioni 25 kwa ajili ya ujenzi wa hospitali ya rufaa katika wilaya ya Ukerewe.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • RC MTANDA AIPONGEZA OFISI YA WAZIRI MKUU KUANZISHA KAMATI ZA MAAFA ZA MIKOA

    November 18, 2025
  • RC MTANDA AWATAKA WATAKWIMU KUTOA TAKWIMU SAHIHI KUCHAGIZA MAENDELEO

    November 18, 2025
  • RAS MWANZA AONGOZA WAOMBOLEZAJI MAZISHI YA ALIYEKUWA MTUMISHI WA MWAUWASA

    November 14, 2025
  • MWANZA YASHIRIKI MAFUNZO KUKUZA USAWA WA KIJINSIA NCHINI MKOANI MOROGORO

    November 13, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.