• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

DKT. JINGU AWATAKA MAAFISA MAENDELEO KUCHANGAMKIA FURSA 30% YA MAKUNDI MAALUM

Posted on: July 3rd, 2025

Katibu Mkuu Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum Dkt. John Jingu amewataka Maafisa Maendeleo ya Jamii nchini kuhakikisha wanachangamkia fursa ya uwepo wa 30% ya Makundi maalum ili yaweze kunufaika.


Dkt. Jingu ameyasema hayo leo julai 03, 2025 wakati akifungua mafunzo kwa Maafisa Maendeleo ya Jamii Mkoa wa Mwanza kuhusu ushiriki wa Makundi maalum katika 30% ya zabuni za umma, na kuwataka kuhakikisha wale watu wote wanaohitaji usaidizi na wenye sifa wanaunganishwa na wadau wanaohusika ikiwemo vitengo vya manunuzi.

“Sisi kaka watendaji jukumu letu kwenye maeneo yetu ni kuhakikisha makundi haya yanakuwepo na yanashughulikia tenda hizi”. Amesema.


Kadhalika, Katibu Mkuu huyo amesema sera ya serikali ni kuwa na uchumi na maendeleo jumuishi na asiwepo mtu wa kubaki nyuma na wote wakiwezeshwa watakuwa wamepambana na umaskini, utegemezi na unyonge.

“Yote haya tukiyafanya tutakuwa tunaiendeleza jamii na tutakuwa tunatimiza adhma yetu”. Ameongeza Dkt. Jingu.


Aidha, Dkt. Jingu amewataka Maafisa maendeleo ya jamii kutoka kila Halmashauri nchini kujitahidi walau kuwa na vikundi visivyoupungua  20 ambavyo vitakua vimesajiliwa kwenye mfumo wa manunuzi na viwe na sifa kushiriki katika mchakato wa manunuzi.


Sambamba na hayo, ameagiza zichukuliwe hatua za makusudi za kuviunganisha vikundi hivyo na fursa zilizopo, fursa za manunuzi kwenye Taasisi mbalimbali za serikali na fursa kwenye maeneo mengine ikiwemo sekta binafsi.


Naye Mkurugenzi Msaidizi idara ya Maendeleo ya jinsia Bi. Juliana Kibonde amesema lengo la mafunzo hayo ni kuhamasisha na kusisitiza umuhimu wa urasimishaji wa makundi maalum na umuhimu wa kufikisha elimu hiyo kwa jamii pamoja na kujenga uelewa katika ushiriki wa makundi maalumu juu ya ununuzi wa umma.


Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • DKT. JINGU AWATAKA MAAFISA MAENDELEO KUCHANGAMKIA FURSA 30% YA MAKUNDI MAALUM

    July 03, 2025
  • MKUU WA WILAYA YA ILEMELA AMTEMBELEA MKUU WA MKOA WA MWANZA

    July 02, 2025
  • TATHMINI NI KIOO – RC MTANDA

    July 02, 2025
  • RC MTANDA AMLILIA AFISA UTAMADUNI AGNES

    July 02, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.