• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

HALMASHAURI ZATAKIWA KUWACHUKULIA HATUA WAZAZI WANAOKIUKA KANUNI ZA MALEZI

Posted on: September 10th, 2025

Katibu Tawala wa Mkoa wa Mwanza Bw. Balandya Elikana amezitaka Halmashauri za Mkoa wa Mwanza kuwachukulia hatua wazazi na walezi ambao wanakiuka sheria na kanuni za malezi ya watoto ikiwemo kuruhusu watoto kwenda mtaani.

Bwana Balandya ametoa rai hiyo leo tarehe 10 Septemba, 2025 wakati akihutubia katika hafla fupi ya kuwatunukia vyeti wahitimu 165 kutoka kwenye vituo vya kulea watoto ambao wamepata mafunzo ya malezi, makuzi na maendeleo ya awali ya mtoto ikiwa ni katika harakati za kumlinda mtoto na ukatili.

Akijibu risala ya washiriki wa mafunzo Bw. Balandya amewataka Maafisa maendeleo ya jamii kuwasaidia wananchi kuzitambua fursa za kuinua kipato na uchumi  zilizopo katka jamii na kuwajengea uwezo ili wajiunge kwenye makundi na kuweza kupata mikopo isiyo na riba.

"Maafisa maendeleo ya jamii mnatakiwa kuwasaidia wananchi kuhakikisha wanatambua na kuzielewa fursa zilizopo katika jamii zetu ambazo zinaweza kuinua kipato chao kwa mfano fursa za mikopo inayotolewa kwa ajili ya kufanya uvuvi wa kisasa wa vizimba." Amesema Bw. Balandya.

Naye, Mganga Mkuu wa Mkoa Dkt. Jesca Lebba amewashukuru wadau waliofadhili mafunzo hayo (RCA) pamoja na wakufunzi na wanafunzi walioungana kwa pamoja kuhakikisha wanapata stadi za kuwalinda watoto na jamii na kwamba wahakikishe wanafikisha elimu hiyo kwa kundi kubwa zaidi la wazazi na walezi ambao hawakupata.

Kwa upande wake mwakilishi kutoka shirika lisilo la kiserikali la Railway Children Afrika (RCA) Bw. Renatus Fuastine wamelenga kuwafikia walezi wa watoto wenye umri wa kuanzia miaka 0-8 ambao wameramani kuona watoto wanaishi kwenye familia zao na sio kuishi mtaani kwa kuwafikia wazazi kwenyw jamii na kuwapa elimu.

"Tuna matumaini walezi mliopata mafunzo haya mtawafikia wazazi na walezi wengi zaidi ambao hawakupata mafunzo haya ili muweze kuwapa elimu hii ili tuondokane na ukatili wa watoto na wanawake, nyie mmeshakua mabalozi na tunawategemea na kwa siku za usoni tutawafikia wengine nje ya Nyamagana na Ilemela", amesisitiza.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • RC MTANDA AKABIDHI MAGARI YA BILIONI 1.3 KWA JESHI LA POLISI

    September 12, 2025
  • SERIKALI KUENDELEA KUTATUA CHANGAMOTO ZA WATUMISHI NCHINI

    September 11, 2025
  • MAJALIWA AAGIZA KUIMARISHWA ZAIDI SEKTA YA UFUATILIAJI, TATHMINI NCHINI

    September 11, 2025
  • NSSF WAFANYA ZIARA YA UWEKEZAJI MWANZA

    September 10, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.