• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

KATIBU SEKRETARIETI YA AJIRA AWAONYA WAOMBAJI KAZI DHIDI YA MATAPELI, AWAHAKIKISHIA HAKI NA USAWA KATIKA AJIRA

Posted on: December 20th, 2025

Katibu wa Ofisi ya Rais, Sekretarieti ya Ajira katika Utumishi wa Umma, Bw. Mick Kiliba amewatahadharisha waombaji wa ajira nchini dhidi ya vitendo vya utapeli vinavyoendelea kujitokeza, huku akisisitiza kuwa hakuna mtu, mtumishi au msimamizi wa usaili mwenye uwezo wa kumpatia msailiwa ajira kwa njia ya mkato.

Akizungumza wakati wa ufuatiliaji wa zoezi la usaili kwa waombaji wa ajira katika Mkoa wa Mwanza, Katibu huyo amesema ajira zote zinazotangazwa na Serikali hazijamlenga mtu binafsi, kundi au eneo fulani, bali ni kwa Watanzania wote wenye sifa na vigezo, ambapo nafasi hutolewa kwa misingi ya ushindani wa haki.

Amesema kuwa Serikali imeweka mfumo madhubuti wa kuhakikisha mchakato wa ajira unazingatia haki, sheria, miongozo na utu, hivyo hakuna sababu ya waombaji kujihusisha na vitendo vya kutoa au kupokea fedha kwa lengo la kupata ajira.

“Juzi mzazi mmoja alifika ofisini Sekretarieti ya Ajira Dodoma akitokea Mkoa wa Mara, akilalamika kutapeliwa shilingi milioni nne kwa kuahidiwa ajira. Nashangaa mtu anatoa fedha ili apate ajira, kwani mwisho wa siku atatapeliwa na ajira hataipata kwa sababu hakuna mwenye uwezo wa kumpatia mtu ajira,”amesema Katibu huyo.

Katibu huyo ameeleza kuwa kwa sasa mchakato wa ajira unatekelezwa kwa kutumia mfumo wa kidijitali, ambapo hatua zote muhimu ikiwemo upakiaji wa vyeti, ujazaji wa taarifa binafsi na usaili wa kuandika hufanyika kupitia mtandao, isipokuwa hatua ya usaili wa mahojiano kwa waombaji watakaofaulu hatua za awali.

Katika kuondoa wasiwasi kwa waombaji, Kiongozi huyo amesema mfumo huo ni rafiki na rahisi kutumia, na kuwahimiza wale wasio na ujuzi wa kutumia kompyuta kutoona aibu kuuliza au kuomba msaada wanapokumbana na changamoto.

Kwa upande wake, Katibu Tawala Msaidizi Sehemu ya Utawala na Usimamizi Rasilimali Watu kutoka Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Bw. Daniel Machunda, amesema maandalizi ya usaili yamezingatia kikamilifu masuala ya usalama, utulivu na uwepo wa wataalamu wa kutosha.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • MRADI WA UMWAGILIAJI IBANDA–IGAKA WA BILIONI 35 HAUTASIMAMA – SILINDE

    January 10, 2026
  • RC MTANDA MGENI RASMI MECHI YA KIRAFIKI SIMBA VS PAMBA MWANZA

    January 10, 2026
  • BODI YA BARABARA MWANZA YATAKIWA KUSIMAMIA UBORA NA MATUMIZI SAHIHI YA FEDHA

    January 08, 2026
  • MHE. KUNDO KUKAGUA MIRADI YA MAJI MWANZA KWA SIKU TATU

    January 07, 2026
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.