• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

Makatibu wa Afya nchini wapewa Rai ya Ukusanyaji Mapato

Posted on: May 19th, 2023

*Makatibu wa Afya nchini watakiwa kupanua wigo wa Ukusanyaji Mapato*


Katibu Tawala Mkoa wa Mwanza Ndugu Balandya Elikana amewataka Makatibu wa Afya Nchini kusimamia Mifumo ya Ukusanyaji Mapato kwenye maeneo yao ya kazi ili kuimarisha taasisi zao kwenye sekta ya Rasilimali fedha.

Balandya amesema hayo leo Mei 19, 2023 jijini Mwanza wakati akifunga Mkutano Mkuu wa Mwaka wa Chama cha Makatibu wa Afya Tanzania ambao umefanyika Mkoani humo kwenye ukumbi wa Gold Crest kuanzia Mei 16-19, 2023.

"Ni muhimu sana kusimamia vizuri mifumo ili iweze kutuongezea mapato kwani tukijiimarisha kwenye eneo hilo kutasaidia kupata Rasilimali fedha zitakazosaidia kwenye utekelezaji wa majukumu badala ya kusubiri fedha kutoka serikali kuu." Amesisitiza Katibu Tawala.

Vilevile, ametoa rai kwa kundi hilo kwenda kutoa elimu ya mfuko wa fidia kwa wafanyakazi kwa watumishi walio kwenye maeneo yao ili kurahisisha uratibu wa shughuli za mfuko huo na kusaidia watumishi wanapoumia kazini kupata haki zao.

Hata hivyo, amewataka kwenda kusimamia upatikanaji wa takwimu sahihi katika kutoa maamuzi ili maamuzi yoyote yatokane na takwimu sahihi ili kuweka uhalisia wa ushughulikiaji wa masuala mbalimbali.

"Nina imani kuwa ndani ya hizi  siku mlizokuwepo hapa mmepeana hamasa na chachu ya kuongeza bidii na kuwezesha utoaji wa huduma bora hivyo twendeni tukaboreshe huduma za takwimu kwenye maeneo yetu." Balandya.

"Nina uhakika maazimio mliyojiwekea ndani ya siku tano za Mkutano huu mtakwenda kuyatekepeza kwa vitendo ili kuongeza ufanisi kwenye huduma" Amesema

Kaimu Mganga Mkuu Mkoa wa Mwanza Bi Claudia Kaluli wakati akimkaribisha Mgeni Rasmi.

Naye, Mwenyekiti wa Chama cha Makatibu wa Afya Bi. Juliana Mawala ametumia wasaa huo kuwaasa Makatibu wa Afya kwenda kujituma kwa dhati ili kuhakikisha wananchi wanahudumiwa ipasavyo na pia ameshukuru Uongozi wa Mkoa kwa ushirikiano.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.