Swahili
  • English
  • Swahili
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

MCHAKATO WA KULIGAWA JIMBO LA MAGU WAANZA RASMI-TUME YA UCHAGUZI

Posted on: April 23rd, 2025

MCHAKATO WA KULIGAWA JIMBO LA MAGU WAANZA RASMI-TUME YA UCHAGUZI


Mwenyekiti wa Tume huru ya Taifa ya Uchaguzi Mhe. Jaji Jacobs Mwambegele leo Aprili 23,2025 ametangaza rasmi kuanza mchakato wa kuligawa jimbo la Magu kwa kufuata miongozo yote ya kikatiba na ya Tume hiyo.

Akizungumza na wadau wa uchaguzi kwenye ukumbi wa Ofisi ya Mkuu wa wilaya ya Magu, Mwenyekiti huyo amesema mchakato unaofanywa na Tume yake ni kuja kujiridhisha kutokana na maombi yaliyofanyika  kuanzia ngazi ya wilaya hadi Mkoa kabla ya kutangaza rasmi jimbo jipya lililopendekezwa  la Sanjo.

"Ndugu wadau mliofika hapa naomba tuelewane vizuri msianze kutoka hapa na kusema tayari Jimbo limegawanywa hapana, tume hii inafanya kazi kwa kufuata miongozo ya katiba ya nchi yetu na vifungu vya tume, tumekuja kujiridhisha kwa kuwasikia kile mlichoamua kwa kufuata vikao halali na sisi pia kupita kulikagua jimbo husika", Mhe.Mwambegele.

Aidha, ameongeza kuwa Tume imetimiza matakwa ya kanuni ya 18 ya kanuni ya Tume hiyo ya mwaka 2024 ya kutembelea majimbo yote likiwemo la Magu yaliyoomba kugawanywa au kubadilishwa majina.

Kwa upande wake, Kaimu Mkurugenzi wa tume hiyo bwana Greyson Okado akiwaapisha wadau hao kwenye maombi yaliyotumwa amebainisha Jimbo la Magu lina zaidi ya wakazi laki nne, jumla ya kata 25 na endapo ombi lao litakubaliwa Jimbo la Magu litabaki na kata 14 na Jimbo la Sanjo liwe na kata 11 na kila Jimbo litabaki na wakazi zaidi ya laki mbili.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • WAZIRI MKUU AWATAKA WANAMALYA KUCHANGAMKIA FURSA YA CHUO CHA MICHEZO

    May 18, 2025
  • NIA YA SERIKALI KILA MWANANCHI AUNGANISHIWE MAJI NYUMBANI KWAKE - WAZIRI MKUU

    May 18, 2025
  • MAKUZI YA AWALI YA MTOTO MSINGI WA UJENZI WA TAIFA IMARA - RAS BALANDYA

    May 16, 2025
  • RC MTANDA AWAKARIBISHA MWANZA WANAFUNZI KUTOKA UGANDA

    May 15, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.