• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

MHE. KUNDO KUKAGUA MIRADI YA MAJI MWANZA KWA SIKU TATU

Posted on: January 7th, 2026

Naibu Waziri wa Maji, Mhe. Kundo Mathew (Mb) amesema Serikali itaendelea kutekeleza miradi mbalimbali ya maji nchini kwa lengo la kuwaondolea wananchi adha ya ukosefu wa rasilimali hiyo muhimu kwa maendeleo ya kijamii na kiuchumi.

Mhe. Kundo ametoa kauli hiyo mapema leo mkoani Mwanza alipofika katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa kwa ajili ya salamu za kikazi, ikiwa ni sehemu ya ziara yake ya siku tatu ya kukagua utekelezaji wa miradi ya maji inayosimamiwa na Mamlaka za RUWASA, MWAUWASA na SEUWASA katika wilaya mbalimbali za mkoa huo.

Amesema Wizara ya Maji haiishii tu katika utekelezaji wa miradi mipya, bali pia inafanya mapitio ya vyanzo vya maji ili kubaini uwezo wake, kusimamia matumizi sahihi na kuhakikisha vyanzo hivyo vinalindwa ili viendelee kutoa huduma kwa wananchi kwa muda mrefu.

Aidha, Mhe. Kundo amesema wizara imeweka mikakati madhubuti ya kuzuia upotevu wa maji kwa kukomesha vitendo vya wizi wa maji, uchepushaji na uchakavu wa miundombinu, hatua ambayo inalenga kulinda rasilimali hiyo na kuhakikisha maji yanayozalishwa yanatumika ipasavyo.

Akimkaribisha Naibu Waziri huyo Kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Mkuu wa Wilaya ya Ukerewe Mhe. Christopher Ngubiagai ameipongeza Wizara ya Maji kwa kutekeleza jumla ya miradi mikubwa 75 ya maji vijijini yenye thamani ya zaidi ya shilingi bilioni 155, pamoja na mradi wa maji wa thamani ya shilingi bilioni 48 unaotekelezwa maeneo ya mjini.

Amesema mradi huo wa mjini ukikamilika utawezesha kumaliza changamoto ya upatikanaji wa maji katika maeneo yenye miinuko, hali ambayo kwa muda mrefu imekuwa kero kwa wakazi wa maeneo hayo.

Halikadhalika, Mhe. Ngubiyagai amewasilisha kilio cha wananchi zaidi ya laki moja wanaonufaika na Mradi wa Maji wa Kiguru–Usagara–Sumve wenye thamani ya shilingi bilioni 41, akiomba utekelezaji wake uharakishwe ili wananchi hao waondokane na adha ya ukosefu wa maji safi na salama.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • MRADI WA UMWAGILIAJI IBANDA–IGAKA WA BILIONI 35 HAUTASIMAMA – SILINDE

    January 10, 2026
  • RC MTANDA MGENI RASMI MECHI YA KIRAFIKI SIMBA VS PAMBA MWANZA

    January 10, 2026
  • BODI YA BARABARA MWANZA YATAKIWA KUSIMAMIA UBORA NA MATUMIZI SAHIHI YA FEDHA

    January 08, 2026
  • MHE. KUNDO KUKAGUA MIRADI YA MAJI MWANZA KWA SIKU TATU

    January 07, 2026
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.