• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

MWANZA NI SEHEMU SAHIHI YA UWEKEZAJI - RC MTANDA

Posted on: April 10th, 2025

MWANZA NI SEHEMU SAHIHI YA UWEKEZAJI - RC MTANDA


Serikali ya Mkoa wa Mwanza imewakaribisha na kuwahakikishia ushirikiano wa dhati Wawekezaji na Wafanyabiashara wote wanaotamani kuja kufanya biashara na uwekezaji katika Mkoa wa Mwanza ikiwa ni kwa mustakabali wa kukuza biashara na uchumi wa Mkoa na Taifa kwa ujumla.

Kauli hiyo imetolewa leo Aprili 10, 2025 na Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Said Mtanda alipokuwa akifungua Semina ya uhamasishaji wa masuala ya ushindani yenye lengo la kumlinda mlaji wa bidhaa bandia kwa wazalishaji wa Jiji la Mwanza, ambapo amewashukuru Tume ya ushindani (FCC) kwa kufungua Ofisi ya Kanda Mkoani Mwanza.

Mkuu wa Mkoa amesema kwa kufungua Ofisi katika Mkoa wa Mwanza inaongeza juhudi, kuleta huduma karibu na wananchi na kufanya utekelezaji wa majukumu kwa mujibu wa sheria hususani katika masuala ya ushindani, udhibiti wa bidhaa bandia na kumlinda mlaji kwa ujumla.

“Kwa mujibu wa Sensa ya watu na makazi iliyofanyika tarehe 23 Agosti, 2022 Mkoa wa Mwanza una jumla ya watu 3,699,872 Idadi hii ya watu ni fursa katika masoko na biashara ukizingatia pia Mkoa wa Mwanza ni wa pili kwa idadi ya watu ukitanguliwa na Mkoa wa Dar es Salaam”.

Aidha Mkuu wa Mkoa amesema kiuchumi Mkoa wa Mwanza unachangia kwenye pato la Taifa (GDP) kwa Trilioni 13.59. ukiwa ni Mkoa wa Pili kwa kuchangia kwa asilimia kubwa kwenye pato la Taifa, ambapo Mkoa wa Mwanza unachangia kwa asilimia 7.2.

Sambamba na hayo Mhe. Mtanda ameeleza kuwa uchumi wa Mkoa wa Mwanza unachangiwa na Kilimo 75% (mazao, mifugo na misitu); huduma 10% (biashara, hoteli, usafirishaji, mawasiliano, taasisi za kifedha, kodi za pango, elimu, afya, na utawala); Uvuvi 7% na viwanda na ujenzi 8% (madini, umeme, maji, ujenzi na uzalishali).

“Nimeelezea uchumi wa Mkoa kwa uchache na takwimu si kwa sababu mimi ni bingwa wa Takwimu, hapana, bali nimefanya hivyo ili muweze kupata picha halisi ya uchumi wa Mkoa lengo likiwa mkiwa kama sekta ya biashara kwa pamoja muone namna bora ya kuzitumia vizuri fursa za kiuchumi zilizopo”.

Kadhalika Mkuu wa Mkoa amewaomba FCC haswa walio katika Kanda ya Mwanza kushirikiana pamoja na kwa ukaribu ili kuhakikisha masuala ya kiushindani yanasikilizwa na yanatatuliwa kwa wakati na wananchi wanapewa elimu zaidi kuhusu masuala ya ushindani, kumlinda mlaji na mapambano dhidi ya bidhaa bandia.

kabla ya kufungua semina hiyo Mkuu wa Mkoa amewataka wafanyabiashara waliopata fursa ya kuhudhuria semina hiyo kwenda kuitumia vizuri elimu watakayopata na kuwa mabalozi wazuri wa FCC katika kuwaelimisha wafanyabiashara, wazalishaji wenye viwanda wengine na wananchi kwa ujumla ambao hawakupata fursa ya kuhudhuria mafunzo hayo.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • MWANZA, SIMIYU ZANG'ARA UTAMILIFU DARASA LA SABA KANDA YA ZIWA

    May 30, 2025
  • RAS MWANZA AZINDUA RASMI MRADI WA KUPAMBANA NA UGONJWA WA SELI MUNDU

    May 30, 2025
  • WAANDISHI WA HABARI MWANZA WAPIGWA MSASA MIKAKATI YA KUTOKOMEZA WATOTO WA MITAANI

    May 29, 2025
  • RAS MWANZA AWATAKA VIONGOZI WA UMMA KUDUMISHA NIDHAMU NA UFANISI KAZINI

    May 26, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.