• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

MWANZA YASHIRIKI MAFUNZO KUKUZA USAWA WA KIJINSIA NCHINI MKOANI MOROGORO

Posted on: November 13th, 2025

Wataalamu kutoka Mkoa wa Mwanza wakiongozwa na Afisa Maendeleo ya Jamii wa Mkoa huo Bi. Janeth Shishila wapo Mkoani Morogoro katika Mafunzo ya siku mbili ya Mradi wa Advancing Gender Equality in Tanzania (PAMOJA) unaolenga kukuza Usawa wa Kijinsia nchini.

Mradi huo unaotekelezwa kwa kushirikiana kati ya Ofisi ya Rais -TAMISEMI na Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum, Wizara ya Fedha pamoja na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar kwa mkopo wenye masharti nafuu kutoka Benki ya Dunia utadumu kwa kipindi cha mwaka 2024/25 hadi 2028/29.

Mafunzo haya yatafanyika kwa siku mbili yaani leo tarehe 13-14 Novemba 2025 katika ukumbi wa Chuo Kikuu cha Jordan ukiikutanisha mikoa ya Arusha, Geita, Kagera, Mara, Mwanza, Rukwa, Shinyanga, Simiyu, Singida na Tabora na halmashauri 40.

Mratibu wa Mradi wa PAMOJA kutoka Wizara ya Maendeleo Ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalumu Bi. Adventina Kato ametoa rai kwa wataalamu hao kutekeleza mradi kwa kufuata miongozo ya mradi ili kujihakikishia kufikia malengo ya kimkataba baina ya serikali na wahisani ambao ni benki ya Dunia.

Mradi huo unatekelezwa kuanzia Julai (Hatua za awali) 2025 kwa miaka mitano kwa thamani ya Dola Milioni 100 ambapo asilimia 87 ni kwa ajili ya Bara na 13 ni za upande wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar na kwamba pamoja na mambo mengine fedha hizo zimeelekezwa zaidi kwenye uwezeshaji wanawake kiuchumi.

Aidha, amebainisha kuwa kwa siku za mbeleni mradi huo unaotarajiwa kuzinduliwa rasmi mwanzoni mwa mwezi Disemba mwaka huu halmashauri tano zinatarajiwa kuongezwa ikiwemo halmashauri ya wilaya ya Ukerewe kutoka mkoani Mwanza ambayo kwa sasa haijajumuishwa.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • RAS BALANDYA AMEWATAKA WAHITIMU IFM KUWA MABALOZI WAZURI WA CHUO CHAO

    December 06, 2025
  • RC MTANDA AWATAKA VIJANA KUCHANGAMKIA FURSA ZINAZOPATIKANA

    December 06, 2025
  • SERIKALI YATENGA FEDHA KUKAMILISHA MIRADI YA MAENDELEO MWANZA - DKT. NCHEMBA

    December 05, 2025
  • DKT. NCHEMBA ATOA POLE KWA WANANCHI WALIOHARIBIWA MALI KUTOKANA NA VURUGU MKOANI MWANZA

    December 05, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.