• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

Mwenge wa Uhuru kukimbizwa Mwanza kwenye Miradi ya Shs Bilioni 18.7

Posted on: July 13th, 2022


Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe Mhandisi Robert Gabriel leo tarehe 12 Julai, 2022 amepokea Mwenge wa Uhuru katika kijiji cha Mwamhembo-Malya wilayani Kwimba ukitokea Mkoani Simiyu ambapo amesema utakimbizwa kwenye jumla ya KM 563 eneo la Nchi kavu na 'Nautical Miles' 86.3 eneo la Maji ziwa Victoria.

Aidha, amemshukuru Mhe Rais Samia Suluhu Hassan kwa kupeleka fedha nyingi kwa ajili ya kutekeleza miradi ya Maendeleo Mkoani humo katika Sekta za Elimu, Afya, Miundombinu na Maji na amebainisha kuwa Mwenge wa Uhuru utaifikia Miradi 52 yenye thamani ya zaidi ya Tshs. Bilioni 18.7 kati ya hiyo 15 itawekewa mawe ya msingi, 29 itazinduliwa, 3 itafunguliwa na 5 itakaguliwa.

"Mwenge wa Uhuru utafanya ukaguzi kwenye miradi ya anuani za makazi inatotekelezwa katika Halmashauri zote ambapo hadi kufikia tarehe 7. 3. 2022 jumla ya nyumba 653,827 zimewekewa namba sawa na asilimia 118.54 hivyo kuvuka lengo lililowekwa. Jumla ya Anuani zilizosajiliwa katika mfumo ni 670,407 ambapo utekelezaji wa Mkoa umekamilika kwa asilimia 102." Amefafanua.

Vilevile, amesema zoezi la uwekaji Nguzo zinazoonesha majina ya Barabara limekua likiendelea vema Mkoani humo na kufikia tarehe 30 Juni, 2022 jumla ya Nguzo zilizotengenezwa ni 31,525 na kufanya Utekelezaji kukamilika kwa asilimia 104.7

Mhe. Mhandisi Gabriel amesema Mkoa huo umeendelea kutekeleza Kaulimbiu ya Mapambano dhidi ya Lishe duni, Mapambano dhidi ya Ugonjwa wa UKIMWI/VVU, na amebainisha kuwa yameendelea kupungua kutoka asilimia 15.1 hadi asimilia 8.1 mwaka hadi mwaka na kwamba vijana wameendelea kuwezeshwa kiuchumi kupitia Mfuko wa Maendeleo ya Vijana.

Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru, Ndugu Sahil Nyanzabala ameziagiza Halmashauri zote nchini kuhakikisha fedha wanazokopeshwa Vijana zinarejeshwa kwa wakati ili ziweze kukopeshwa tena kwa vikundi vingine na kuwasaidia kujikwamua kwenye shughuli mbalimbali kama za Kilimo, ujasiriamali, uvuvi, biashara na ufugaji.

Katika wakati mwingine, Mhe. Mkuu wa Mkoa amemkabidhi Mwenge wa Uhuru Mhe. Johari Samizi, Mkuu wa Wilaya ya Kwimba utakaokimbizwa leo wilayani humo chini ya Kaulimbiu ya Kitaifa 2022 'Sensa ni Msingi wa Mpango wa Maendeleo, Shiriki kuhesabiwa tuyafikie Malengo ya Taifa'..

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.