• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

NIA YA SERIKALI KILA MWANANCHI AUNGANISHIWE MAJI NYUMBANI KWAKE - WAZIRI MKUU

Posted on: May 18th, 2025

NIA YA SERIKALI KILA MWANANCHI AUNGANISHIWE MAJI NYUMBANI KWAKE - WAZIRI MKUU


Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Kassim Majaliwa Majaliwa (Mb.) amesema dhamira ya Serikali ya awamu ya Sita ni kuhakikisha wanasogeza huduma ya maji katika makazi ya wananchi ili mama asibebe tena ndoo kichwani bali mkononi na kuingiza ndani.

Mhe. Waziri Mkuu ameyasema hayo leo Mei 18, 2025 alipokuwa akiwasalimia wananchi wa Hungumalwa Wilayani Kwimba mara baada ya kuzindua mradi mkubwa wa maji na kuwahakikishia wanachi hao uhakika wa kupatikana kwa kipindi chote maji hayo yaliyounganishwa kutoka ziwa victoria.

Aidha, Mhe. Majaliwa amesema Serikali inaendelea kuangalia gharama za uendeshaji na matumizi kupitia jumuiya za watumia maji ili kila mwananchi anaetumia maji alipe gharama za maji kulingana na kiasi anachotumia na kwa gharama nafuu.

“Lengo la Serikali yenu ni kupatikana kwa huduma ya maji safi na salama kwa wananchi wa Hungumalwa kwa 100%”.

Awali, akisoma Taarifa ya mradi huo Meneja wa Wakala wa Maji na Usafi wa Mazingira Vijijini (RUWASA) Mkoa wa Mwanza Mhandisi Godfrey Sanga amesema Mradi huo umetekelezwa na Mkandarasi Emirate Builders Company Ltd na kusimamiwa na wataalam wa RUWASA ambapo gharama ya mkataba ni Sh. 11,004,143,176.82 na ulianza kutekelezwa mwezi machi 03, 2022 na kukamilika agosti 15, 2024.  

“Mpaka sasa kazi zote zimekamilika zenye thamani ya Sh. 10,803,026,273.14 na kubaki na salio katika mkataba la Sh. 201,116,903.68”. Mhandisi Sanga.

Mradi huo wa Hungumalwa unahudumia jumla ya wakazi 24,349 wa vijiji vya Hungumalwa, Buyogo, Ilula na Kibitilwa ambapo umeongeza asilimia ya upatikanaji Maji katika wilaya ya Kwimba kutoka asilimia 77.3 kufikia 79.4.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • WAZIRI MKUU AWATAKA WANAMALYA KUCHANGAMKIA FURSA YA CHUO CHA MICHEZO

    May 18, 2025
  • NIA YA SERIKALI KILA MWANANCHI AUNGANISHIWE MAJI NYUMBANI KWAKE - WAZIRI MKUU

    May 18, 2025
  • MAKUZI YA AWALI YA MTOTO MSINGI WA UJENZI WA TAIFA IMARA - RAS BALANDYA

    May 16, 2025
  • RC MTANDA AWAKARIBISHA MWANZA WANAFUNZI KUTOKA UGANDA

    May 15, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.