• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

RAIS SAMIA ATOA ZAWADI ZA SIKUKUU YA KRISMAS KWA WATOTO YATIMA NA WENYE MAHITAJI MAALUM MWANZA

Posted on: December 25th, 2024

RAIS SAMIA ATOA ZAWADI ZA SIKUKUU YA KRISMAS KWA WATOTO YATIMA NA WENYE MAHITAJI MAALUM MWANZA


Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Said Mtanda amekabidhi zawadi za Sikukuu ya Krismas kwa niaba ya Mhe. Rais Samia Suluhu Hassan kwa watoto yatima na wenye mahitaji maalum katika vituo vya malezi vya Tawfiq kilichopo Mhandu-Nyamagana na TCRC-Nyasaka Ilemela.

Akizungumza katika nyakati tofauti baada ya kukabidhi zawadi hizo Mhe. Mtanda amemshukuru Mhe. Rais kwa kuamua kusherehekea Sikukuu pamoja na watoto kwa kuwakumbuka kwa zawadi ili watoto hao wale na kunywa na kufurahia siku kuu hiyo.

"Kwa zawadi hizi namshukuru sana Mhe. Rais kwani watoto hawa leo watafurahia na kutambua kuwa wanao walezi pamoja na kwamba hawana wazazi, watakula na kunywa kwa furaha kwani amewakimbilia yatima na wajane hawa." Mhe. Mtanda.

Aidha, amebainisha kuwa serikali itaendelea kushirikiana na vituo vya malezi ya watoto wakati wote kwani lengo la wenye vituo ni jema na la kiutu sana hivyo ni lazima serikali iwaunge mkono.

"Watu wa Ustawi wa jamii endeleeni kusimamia vituo hivi na kuwapa miongozo ili wapatiwe elimu na kukomesha matendo ya ukatili wa watoto na kijinsia katika maeneo ya vituo vya malezi." Amesisitiza Mkuu wa Mkoa.

"Kituo hichi kinajumuisha watoto yatima na wenye wazazi lakini wanaotoka kwenye mazingira magumu, kimesajiriwa mwaka 2019 na kwa sasa kina watoto 25 na tunafuata miongozo kutoka kwa serikali ikiwemo kuwapatia Elimu." Salum Juma Khatib, Mkuu wa Kituo cha Tawfiq.

Pamoja na zawadi hizo za Maharage, Mbuzi, Mchele, Sukari, Sabuni za vipande na za unga, Mafuta ya kupikia, Soda, Juice ambavyo kwa pamoja vina thamani ya zaidi ya Tshs. Milioni 2, Mhe. Mkuu wa Mkoa binafsi amekichangia kituo cha Tawfiq Tshs. Milioni 1.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.