• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

RAIS SAMIA AWATAKA WANANCHI WA MKOA WA MWANZA KUTANGULIZA UZALENDO NA KUILINDA MIRADI

Posted on: June 14th, 2023

RAIS SAMIA AWATAKA WANANCHI WA MKOA WA MWANZA KUTANGULIZA UZALENDO NA KUILINDA MIRADI


*Amtaka Mtendaji Mkuu TANROADS kulisimamia kikamilifu liwe na ubora*


*Awahakikishia wananchi kasi ya kuwaletea Maendeleo*


*Ashukuru kwa mapokezi makubwa tangu amewasili Mwanza*


*Aahidi kukuza uchumi Watanzania  kwa kupitia miradi *


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.Dkt. Samia Suluhu Hassan amewataka wananchi wa Mkoa wa Mwanza kutanguliza uzalendo katika mradi ya maendeleo na kuepukana na aina yoyote ya wizi ambao utarudisha nyuma kasi ya umaliziaji wake.

Akizungumza leo na wananchi Wilayani Misungwi mara baada ya kupata taarifa ya mradi wa Daraja la Kigongo- Busisi, Dkt.Samia amesema huo unakuja kukuza uchumi wa Taifa na wananchi wa eneo hilo hivyo wana kila sababu ya kuulinda kwa faida yao.

"Ndugu zangu wananchi nimepita kidogo hapa kuona maendeleo ya mradi huu ambao sasa umefikia zaidi ya asilimia 70 kabla ya kukamilika,nimefarijika ila nimesikia kuna ka-mkono wa udokozi wa vifaa,kemeeni hilo na wacheni," amesisitiza Mhe.Rais.

Aidha, amemtaka Mtendaji Mkuu wa wakala wa barabara TANROADS, Mhandisi Mohamed Besta kuhakikisha Daraja hilo linakuwa na ubora kwa kusimamia kila hatua na vipimo vyote vifanywe kwenye maabara za Serikali na siyo kufanywa na Mkandarasi pekee.

"Mhe.Rais Daraja hili linalojulikana kama JP Magufuli lenye urefu wa kilomita 3 limegharimu Shs bilioni 716.33 na hadi sasa Mkandarasi CCECC Construction kutoka China amelipwa Shs bilioni 368.67 na tumefikia asilimia 75 ya utekelezaji na itapitiwa na barabara kuu ya Usagara-Sengerema hadi Geita,"  Mhandisi Besta

Mtendaji huyo Mkuu wa wakala wa barabara nchini amebainisha mradi huo wa Daraja pia umekuwa ni darasa kwa wahandisi wa hapa nchini kutokana na kuwekwa katika kila eneo kwa lengo la kuongezewa ujuzi.

"Mhe.Dkt.Samia kwa niaba ya wananchi wa Jimbo la Misungwi tunaendelea kukushukuru kwa kuonesha kwa vitendo kasi ya maendeleo,miradi mingi imefanyika Jimboni kwangu kuanzia Sekta ya afya na elimu,na wananchi wa Misungwi wamefurahi sana kutujengea barabara ya Mwanangwa hadi Misasi kwa kiwango cha lami",Mhe.Alexander Mnyeti,Mbunge wa Misungwi

Akikagua Ujenzi wa Meli ya MV Mwanza inayojengwa kwa Bilioni 109 kwenye Bandari ya Mwanza Kusini Mhe. Rais amewataka watanzania kufanya kazi kwa bidii ili ukamilifu wa Meli hiyo inayotarajia kubeba zaidi ya Watu 1200 na Tani 400 za Mizigo kwa wakati mmoja usaidie kufungua uchumi wa nchi kwa kubeba mizigo.

"Tunakwenda kuwafungua watanzania kiuchumi, tunajenga Meli, Bandari na Reli viende sambasamba na sisi kufanya kazi kwa bidii ili kila kinachozalishwa kwenye mashamba yetu kiende sokoni na kazi hii inafanywa kwenye kila kona ya nchi hii," Amesisitiza Rais Samia.


Naye, Mkurugenzi wa Kampuni ya Huduma za Meli (MSCL) Erick Hamissi amesema meli hiyo imeshajengwa kwa zaidi ya asilimia 80 na kwamba mkandarasi ameshalipwa fedha hadi hatua hiyo na inatarajiwa kukamilika Mwezi Agosti 2023 na watanzania zaidi ya 200 wameajiriwa hapo wakiongozwa na wataalamu Wakorea 13 tu.

Katika wakati mwingine, Mhe. Rais  amewapongeza NSSF kwa Mradi mzuri wa Hoteli ya Kisasa ambayo italeta Tija mkoani humo na akawataka kupanua huduma hiyo kwenye majiji mengine Nchini.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.