• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

RAS BALANDYA AWAKARIBISHA VIONGOZI WA PPRA MWANZA

Posted on: June 18th, 2024

RAS BALANDYA AWAKARIBISHA VIONGOZI WA PPRA MWANZA


Katibu Tawala Mkoa wa Mwanza Bw. Balandya Elikana leo Juni 18, 2024 amewapokea na kufanya nao mazungumzo Mkoani Mwanza Bodi ya Wakurugenzi na Menejimenti kutoka Mamlaka ya Udhibiti Ununuzi wa Umma (PPRA) ambao wako Mkoani humo kwa ziara ya kikazi ya kukagua na kutembelea miradi ya kimkakati inayotekelezwa.

Balandya amesema kama Viongozi wa Mkoa wanatambua mchango mkubwa unaofanywa na PPRA katika nchi kwa kuzingatia kuwa takribani 80% ya bajeti ya Serikali ni ununuzi wa umma.

Aidha  ameipongeza Bodi na Menejimenti hiyo kwa usimamizi mzuri wa mfumo wa usimamizi wa Ununuzi wa Umma Kielektroniki (Nest), kwani umesaidia na kuongeza uwazi pamoja na uwajibikaji.

"Shughuli zote za manunuzi ya umma zinafanyika kupitia mfumo huu wa Nest, nina imani tukiendelea kuutumia italeta mapinduzi makubwa katika sekta nzima ya manunuzi ya umma".

Kadhalika Mtendaji huyo wa Mkoa ameishukuru Serikali ya awamu ya sita chini ya Rais Dkt. Samia kwa kuendeleza miradi yote mikubwa ya kimkakati katika Mkoa wa Mwanza, pia ameishukuru PPRA kwa kukubali kufanya na kuidhinisha manunuzi katika miradi yote hiyo ikiwemo mradi wa daraja la Kigongo-Busisi, Soko la Kisasa lililopo mjini kati, ujenzi wa Meli ya MV. Mwanza Hapa Kazi Tu, na upanuzi wa uwanja wa ndege wa Mwanza

Naye Mkurugenzi Mkuu wa PPRA Bw. Eliakim Maswi amesema kwa sasa wana sheria mpya wanayoitumia ambapo Serikali imeamua kuwapa kipaumbele makampuni ya ndani katika kusimamia na kutekeleza miradi mbalimbali ya kimkakati na maendeleo ikiwa na adhma ya kuhakikisha kuwa inayalea makampuni ya ndani.

"Kwa sheria yetu hii mpya, sasa siyo kila miradi mikubwa wapewe watu au makampuni kutoka nje, tunataka pia makampuni ya ndani yakue, mabadiliko makubwa yamefanyika chini ya Rais wetu Dkt. Samia na yataleta tija katika kuyakuza makampuni yetu ya ndani". Amesema Maswi.

Wakati huo huo Katibu Tawala wa Mkoa wa Mwanza Bw.Balandya Elikana mapema leo Ofisini kwake amefanya mazungumzo na Makamanda kutoka Jeshi la Zimamoto na Uokoaji ambao wapo Mkoani humo kwa maandalizi ya sherehe za uvulishwaji nishani kwa Maofisa wake na askari siku ya kesho

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.