• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

RAS MWANZA ATAKA FEDHA ZA LISHE ZITUMIKE KWA KUFUATA MUONGOZO WA MKATABA

Posted on: November 5th, 2025

Kaimu Katibu Tawala Mkoa wa Mwanza Ndg. Henry Mwaijega ametoa rai kwa Halmashauri kuhakikisha wanatumia fedha za lishe kwa ajili ya kuwahudumia watoto wa shule na makundi yaliyoainishwa kwenye muongozo ili kuleta maana ya mkataba wa lishe.

Ametoa rai hiyo leo tarehe 05 Novemba, 2025 kwa niaba ya Katibu Tawala wa Mkoa wakati wa kikao cha Utekelezaji wa Mkataba wa Lishe kwa Mwezi Julai hadi Septemba 2025 kilichowakutanisha wataalamu pamoja na makundi ya kijamii kama viongozi wa dini.

Ndugu Mwaijega amesema tatizo la udumavu na utapiamlo, ukondefu au uzito mdogo pamoja na udumavu wanahitaji nguvu ya pamoja kuwaokoa kutoka kwenye makundi hayo kwa kushirikiana jamii na halmashauri kwa kuhakikisha wanawafikia kwa kuwapatia lishe bora.

Mganga Mkuu wa Mkoa Dkt. Jesca Lebba amesema kikao hicho ni cha afya kinga chenye lengo la kukumbusha watumishi na jamii kuepukana na tabia bwete inayopelekea kupata magonjwa yasiyoambukiza pamoja na kupitia utekelezaji wa afua za lishe kwa mujibu wa sheria kwa kila robo kwa ngazi ya mkoa.

Akitoa utekelezaji wa mkataba wa lishe katika kipindi cha robo ya Julai - Septemba 2025, Afisa Lishe Mkoa Bi. Sophia Lugome amesema mkoa huo una udumavu kwa 28% kwa watoto huku Magu na Buchosa wakiongoza hivyo wakurugenzi watendaji wanapaswa kuongeza nguvu katika kuibua na kushughulikia.

Aidha, ametoa wito kwa wataalamu pamoja na viongozi wa dini kushirikiana na ofisi yake kwenda kutoa elimu na kufanya uhamasishaji kwenye redio watapohitajika na amezitaja redio Jembe, Free na Afya kuwa wanashirikia nao sana kwenye utoaji elimu.

Kikao hicho kimeondoka na azimio la kuitaka halmashauri ya Kwimba ambayo ina hali duni kwenye kiashiria cha upangaji wa bajeti na kiasi kinachotolewa kwa ajili afua za lishe kuandikiwa barua ya kuwataka waeleze ni kwa nini wamewasilisha kwa asilimia 4 pekee ili waweze kusaidiwa.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • RC MTANDA AIPONGEZA OFISI YA WAZIRI MKUU KUANZISHA KAMATI ZA MAAFA ZA MIKOA

    November 18, 2025
  • RC MTANDA AWATAKA WATAKWIMU KUTOA TAKWIMU SAHIHI KUCHAGIZA MAENDELEO

    November 18, 2025
  • RAS MWANZA AONGOZA WAOMBOLEZAJI MAZISHI YA ALIYEKUWA MTUMISHI WA MWAUWASA

    November 14, 2025
  • MWANZA YASHIRIKI MAFUNZO KUKUZA USAWA WA KIJINSIA NCHINI MKOANI MOROGORO

    November 13, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.