• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

RAS MWANZA AWAASA WAHITIMU KUTUMIA UBUNIFU, RASILIMALI KUTENGENEZA FURSA

Posted on: November 28th, 2025

Katibu Tawala Mkoa wa Mwanza Bw. Balandya Elikana amewataka wahitimu wa vyuo kutumia ubunifu, ujuzi na mafunzo waliyoyapata kujitengenezea fursa kwa kutumia rasilimali zilizopo ili kujiletea maendeleo.

Amesema hayo leo novemba 28, 2025 kwenye hafla ya kuwapongeza wahitimu (1035) katika ngazi za Astashahada, Stashahada na Shahada wa Chuo Cha Uhasibu Tanzania (TIA) kampasi ya Mwanza iliyopo katika kijiji cha Nyang’homango wilayani Misungwi ambapo alikua mgeni rasmi kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa.

Bw. Balandya amelitaja ziwa Vicroria lenye rasilimali lukuki, migodi na vivutio vya Utalii kama hifadhi ya Saanane kuwa ni miongoni mwa rasilimali zinazohitaji ubunifu ili kujenga fursa kubwa ya kujiendeleza kiuchumi.

“Niwaombe sana, maisha yanahitaji ubunifu, ujuzi na maadili, hivyo basi vyeti mlivyotunukiwa vikawasaidie kubadilisha maisha yenu na jamii. Pia kuweni na moyo wa kujaribu kwani ndio njia pekee ya kusonga mbele kimaisha.” Ameeleza Bw. Balandya.

Aidha, amebainisha kuwa serikali imekuwa ikiwashika mkono wananchi kwa kutoa mikopo kupitia mapato ya ndani ya halmashauri hivyo wahitimu na wananchi wanaalikwa kujiunga vikundi vya ujasiriamali na biashara zingine ili kuchukua mikopo hiyo ili waweze kujiinua kiuchumi na sio kusubiri kuajiriwa pekee.

Akiupongeza uongozi kwa kuendelea kuboresha miundombinu ya chuo kwa kutumia mapato ya ndani hasa ujenzi wa bwalo la chakula litakalobeba watu 600 lililofikia 4% linalotarajiwa kugharimu Tshs. milioni 365 na hosteli itakayobeba wanafunzi 306 iliyofikia 70% huku likitazamiwa kugharimu bilioni 7.2 kwa kutumia mapato ya ndani Bw. Balandya amewasihi kuendelea kujitoa ili kufanya maendeleo yenye tija nchini.

Halikadhalika, amewataka wahitimu hao kuwa na moyo wa uthubutu, uadilifu, na utayari katika kubadilika kwa namna ambavyo dunia inaenda lakini pia kutumia teknolojia za kidigiti kama Akili Mnemba kwa ufasaha.

Naye Afisa Mtendaji Mkuu wa chuo hicho Prof. William Pallangyo amewasihi wahitimu wote kutumia ujuzi na mafunzo waliyoyapata kuhakikisha wanaenda kuishi katika maisha halisi na kulijenga taifa.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • RC MWANZA AKUTANA NA VIONGOZI & WACHUNGAJI WA AICT ASISITIZA AMANI NA MSHIKAMANO

    December 02, 2025
  • TUWE WABUNIFU KWENYE KAZI TUSISUBIRI KUELEKEZWA- RAS BALANDYA

    December 02, 2025
  • RC MTANDA AZITAKA KAMATI ZA USHAURI WA KISHERIA KATIKA MKOA WA MWANZA KUMALIZA NA KUTATUA MIGOGORO YA WANANCHI

    December 02, 2025
  • RAS MWANZA AWAASA WAHITIMU KUTUMIA UBUNIFU, RASILIMALI KUTENGENEZA FURSA

    November 28, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.