• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

RC MAKALLA AZITAKA HALMASHAURI KUWA NA MIPANGO INAYOJIBU KERO ZA WANANCHI MOJA KWA MOJA

Posted on: February 12th, 2024

RC MAKALLA AZITAKA HALMASHAURI KUWA NA MIPANGO INAYOJIBU KERO ZA WANANCHI MOJA KWA MOJA


*Asema ni lazima wananchi wasikilizwe na kutatuliwa shida zao*


*Ataka mipango ya kuongeza wigo wa Ukusanyaji wa Mapato*


*Aagiza udhiti wa Mapato kwa kusimamia mashine za kukusanyia mapato*


*Atangaza Mwezi Machi ni awamu ya usikilizaji kero Jimbo kwa Jimbo *


Mkuu wa Mkoa wa Mwanza CPA Amos Makalla amezitaka Halmashauri kuwa na mipango madhubuti kwenye mpango wa Bajeti itakayojibu moja kwa moja shida za wananchi kupitia huduma zinazotolewa kwa jamii.

Ametoa wito huo mapema leo Februari 12, 2024 kwenye Ukumbi wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wakati akifungua kikao kazi kilichowakutanisha Wakuu wa Wilaya, Makatibu Tawala, Wakurugenzi pamoja na Menejimenti za Halmashauri mahsusi  kujadili maandalizi ya mipango na Bajeti kwa Mwaka 2024/25.

Pamoja na Maagizo sita ya kufuata katika uandaaji wa Bajeti, CPA Makalla amesema ni lazima viongozi na watendaji wadumu kwenye kusikiliza kero za wananchi na kuziwekea mikakati ya kuzitatua mara moja kwani wananchi wengi wamekua na shida mbalimbali za kimaisha wanahitaji kusaidiwa.

"Nimefurahi kwamba nimepata majibu yaliyofanyiwa kazi kutoka kwenye kila wilaya kupitia ziara yangu niliyoifanya kwenye kila Wilaya, na ndio maana wamekuja viongozi wakuu wa nchi lakini hakukua na mabango ya malalamiko hiyo ni faida ya usikilizaji wa kero zao na kuzitatua." CPA Makalla.

Aidha, Mhe. Mkuu wa Mkoa amefafanua kuwa katika kuhakikisha wananchi wanasikilizwa na kujibiwa vema kero zao ni vizuri wakapewa majibu kwa maandishi kwani inakua rahisi kwenye ufuatiliaji wa kero zao zilizobaki pamoja na kuweka kumbukumbu vizuri juu ya zoezi hilo.


Katibu Tawala Mkoa Balandya Elikana ametumia wasaa huo kuitaka Sekretarieti ya Mkoa na Menejimenti za Halmashauri na kuhakikisha katika upangaji wa Bajeti wanazingatia msingi unaoleta tija kwa wananchi wanaowatumikia pamoja na kuwa na vyanzo vipya vya mapato ili kupanua wigo wa ukusanyaji.


Aidha, amesisitiza kuzingatia mipango na mikakati ya udhibiti wa fedha za umma kwa kuzingatia matumizi sahihi ya mashine za mifumo pamoja na upelekaji wa fedha za mapato ya ndani kwenye miradi ya maendeleo kwa mujibu wa sheria pamoja na usimamizi dhahiri wa miradi pamoja na upelekaji wa fedha kwa makundi maalum.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.