• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

RC MTANDA AAGIZA HOJA ZA KIMAKOSA KUMALIZWA HARAKA

Posted on: June 17th, 2025

RC MTANDA AAGIZA HOJA ZA KIMAKOSA KUMALIZWA HARAKA


Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Said Mtanda ameitaka Halmashauri ya Jiji la Mwanza kuzimaliza na kuzifunga hoja za Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali ambazo zimetokana na makosa madogo madogo kwa kurekebisha makosa yaliyofanyika ili kuzimaliza hoja hizo.

Mkuu wa Mkoa ameyasema hayo leo juni 17, 2025 wakati akizungumza katika Baraza la Madiwani kuhusu hoja za Mkaguzi na Mdhibiti Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) katika Halmashauri ya Jiji la Mwanza na kuwataka Maafisa Manunuzi na Maafisa Sheria wa Halmashauri kufanya kazi kwa pamoja katika kuzimaliza hoja hizo zilizojitokeza kutokana na makosa.

“Kama jambo lilifanywa au lilikosewa hata kama na watu waliopita kwa bahati mbaya na kupelekea kuibuka kwa hoja, ushauri wangu mliopo ni lazima kuhakikisha mnakaa chini mnaomba maoni ya CAG ya kuona namna ya kufuta hoja hizo”. Amesema Mkuu wa Mkoa.

Endapo nitaendelea kuwa Mkuu wa Mkoa huu wa Mwanza nikija tena katika Baraza la namna hii na nikakautana na hoja za namna hizi kwa kweli hatutaoneana muhali. Amesisitiza Mkuu wa Mkoa.

Kuhusu hoja ya uwepo wa vyumba wazi katika Stendi ya Mabasi Nyegezi, Mkuu wa Mkoa ameitaka Menejimenti ya Jiji la Mwanza kuketi upya na kubadili mpango wa awali na kuja na mpango mpya unaoendana na uhalisia wa muktadha huo.

“Mimi nashauri ni bora kupata kidogo kuliko kukosa kabisa, kama vyumba vingine mlipanga kuweka hoteli na hamna mwekezaji aliyejitokeza msiendelee kusubiri badilisheni mpango” Ameongeza Mkuu wa Mkoa.

Halmashauri ya Jijij la Mwanza ilikuwa na Jumla ya Hoja 84, Kati ya hizo hoja za miaka ya nyuma zilikuwa 45 na hoja za mwaka wa fedha 2023/2024 zilikuwa 39. zilizofungwa baada ya uhakiki ni 35 hivyo hoja zilizobaki hadi sasa ni 49.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • RAS BALANDYA ATAKA MIRADI YA MAENDELEO KUKAMILIKA KWA WAKATI

    June 17, 2025
  • RC MTANDA AAGIZA HOJA ZA KIMAKOSA KUMALIZWA HARAKA

    June 17, 2025
  • RC MTANDA ATOA MIEZI 2 KWA MANISPAA ILEMELA KUTENGENEZA MAGARI YASIYOTEMBEA

    June 17, 2025
  • RAS BALANDYA ATAKA MIKAKATI KUINUA UFAULU WA WANAFUNZI MAGU

    June 17, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.