• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

RC MTANDA AAGIZA USIMAMIZI THABITI WA VITUO VYA AFYA KUONGEZA MAPATO

Posted on: June 30th, 2025

Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Said Mtanda amewakumbusha Wadau wa Afya Wanaohudumiwa na MSD Kanda ya Mwanza kuwa wana jukumu kubwa la kuvisimamia vituo vya kutolea huduma za afya katika maeneo yao ili viweze kukusanya mapato ya kutosha.


Mkuu wa Mkoa ameyasema hayo leo wakati akifungua Mkutano wa mwaka na wadau wa sekta ya afya ambapo amewataka kusimamia mapato yanayotokana na uchangiaji wa huduma za afya ili yaweze kununua bidhaa za afya, sambamba na kusimamia mnyororo wa ugavi wa bidhaa hizo.


Mhe. Mtanda amesema Serikali ya awamu ya Sita chini ya Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan imeendelea kuongeza kiasi cha fedha inayotengwa kwa ajili ya bajeti ya kununulia bidhaa za afya kwa ajili ya vituo vya kutolea Huduma za Afya ili kuboresha utoaji wa huduma za afya.

“Hivyo, kila mmoja ana jukumu la kusimamia matumizi sahihi ya bidhaa za afya ili Kuleta tija kwa wananchi.”


Kwa kutekeleza haya, wananchi watapata huduma bora zaidi katika vito vya kutolea huduma za Afya bila manung’uniko. Ameongeza Mkuu wa Mkoa.

Kupitia mkutano huo Mkuu wa Mkoa pia amewakumbusha wadau wa MSD kupitia Wizara ya Afya, kufanya maoteo ya bidhaa za afya kwa usahihi, weledi na kwa wakati.

Kadhalika, amewakumbusha kusimamia matumizi sahihi ya takwimu za mnyororo wa ugavi ili ziwasaidie kufanya maamuzi sahihi juu ya bidhaa za afya

Katika maeneo yeo.

Mkutano huo wa MSD na wadau wa afya wa Mikoa mitano ya Mwanza, Simiyu, Shinyanga, Mara na Geita wanaohudumiwa na Kanda ya Mwanza una madhumuni ya Kuboresha uhusiano na mawasiliano kati ya MSD na wadau wa Afya katika mikoa ya Kanda ya ziwa.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • RC MTANDA AAGIZA USIMAMIZI THABITI WA VITUO VYA AFYA KUONGEZA MAPATO

    June 30, 2025
  • RC MTANDA AYASHUKURU MAKUNDI MBALIMBALI USHIRIKI ZIARA YA RAIS DKT. SAMIA

    June 30, 2025
  • RC MTANDA ATOA SOMO LA UONGOZI KWA DC MPYA MAGU

    June 30, 2025
  • KAMA TUNAHITAJI KUSONGA MBELE NI LAZIMA KUJIUNGA NA USHIRIKA – RAS BALANDYA

    June 24, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.