Swahili
  • English
  • Swahili
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

RC MTANDA AFUNGA MAFUNZO YA AWALI JESHI LA AKIBA 2024 SENGEREMA

Posted on: November 17th, 2024

RC MTANDA AFUNGA MAFUNZO YA AWALI JESHI LA AKIBA 2024 SENGEREMA


Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Said Mtanda leo 17 Novemba, 2024 amefunga rasmi mafunzo ya awali ya askari wa jeshi la akiba Kimkoa 2024 yaliyofanyika katika shule ya Msingi Ngoma kata ya Igalula Wilayani Sengerema.

Akizungumza baada ya ukaguzi wa gwaride lililofana  pamoja na maonesho mbalimbali Mhe. Mtanda amewapongeza wahitimu hao 111 waliohitimu kwa kulinda nidhamu, utii na subira wawapo kwenye mafunzo na hatimaye kuwa rasmi askari wa jeshi hilo kama kiapo chao kinavyowataka.

Aidha, amewataka kudumu kwenye kiapo cha kutetea uchumi wa nchi kwa kushiriki katika vitendo vya kupambana na maadui ujinga, maradhi na umasikini katika jamii wanayoishi kwa kuchapa kazi na kutoa hamasa kwa wananchi kuwa wazalendo na kujibidiisha katika masomo ili kujipatia maendeleo.

Vilevile, ametoa wito kwa Halmashauri ya Wilaya ya Sengerema kuhakikisha wanawapatia vijana hao mikopo ili wafanye shughuli za ujasiriamali na wawajengee uwezo hatimaye kuunda makundi yatakayokidhi sifa za utoaji wa mikopo kupitia makundi ya vijana, wanawake na wenye ulemavu.

"Katika uchaguzi wa Serikali za mitaa viongozi na wagombea wote nawasihi mkajiepushe na rushwa kwani ni adui wa haki na kiongozi anayepatikana kwa kutoa rushwa hatowahudumia wananchi kwa moyo wote bali atakua ni mtafuta maslahi." Amesema Mhe. Mtanda alopokuwa akizungumzia uchaguzi wa Serikali za Mitaa.

Naye Mshauri wa jeshi la akiba Sengerema Meja Erick Mateni mesema kuwa vijana hao wataimarisha ulinzi katika maeneo yao kutokana na ukakamavu na uzalendo waliopewa kama vile mbinu za kivita, usomaji wa ramani, ujasiriamali, uraia, usalama wa habari, madhara ya rushwa pamoja na kuzima moto.

Wakisoma risala wahitimu hao Lily Simon na Magreth Edward wametoa ombi la kupewa kipaumbele kwenye kazi za ulinzi hususani kwenye mgodi wa Sota Mining pamoja na kupatiwa mikopo kupitia kundi la vijana, wazee na wenye ulemavu katika Halmashauri.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • LENGO LA HOSPITALI ZA WILAYA NI KILA MWANANCHI APATE HUDUMA MAHALI ALIPO - WAZIRI MKUU

    May 19, 2025
  • MITAMBO YA KUOPOA MAGUGUMAJI KUWASILI MWISHONI MWA MWEZI JULAI.

    May 19, 2025
  • WAZIRI MKUU AWATAKA WANAMALYA KUCHANGAMKIA FURSA YA CHUO CHA MICHEZO

    May 18, 2025
  • NIA YA SERIKALI KILA MWANANCHI AUNGANISHIWE MAJI NYUMBANI KWAKE - WAZIRI MKUU

    May 18, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.