• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

RC MTANDA ATOA SOMO LA UONGOZI KWA DC MPYA MAGU

Posted on: June 30th, 2025

Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Said Mtanda amesema nidhamu na kuwa na malengo ni msingi wa kuwa kiongozi mzuri na bora.


Mkuu wa Mkoa ameyasema hayo leo juni 30, 2025 wakati akimuapisha Mkuu wa Wilaya ya Magu Mteule Bi. Jubilate Win Lauwo, ambapo amesema kazi ya Kiongozi ni usimamizi na uratibu wa shughuli za Serikali katika ngazi ya Wilaya.


Mkuu wa Mkoa amesema kiongozi mzuri ni yule mwenye maono na mwenye kusimamia imani yake juu ya wale anaowaongoza, amemtaka Mkuu wa Wilaya ya Magu atambue Wilaya yake inataka nini ameikuta wapi na lazima aweke malengo ya kuifikisha WIlaya hiyo mahali fulani.

“wewe una elimu kubwa, uzoefu wako wa miaka miwili katika Ukatibu Tawala na unajiamini kwa hiyo tunaanini utakwenda kufanya hii kazi kikamilifu”.


Kadhalika Mhe. Mtanda amesema ili uwe Kiongozi hodari lazima kuwa jasiri wa kuhakikisha unasimamia maono, maamuzi, na msimamo sahihi kuhusu ukweli maana ndio msingi bora wa uongozi.

“Ukishakubali kila unachoambiwa wewe unakuwa kiongozi ambaye unaendeshwa lazima uwe na msimamo, usiruhusu hilo”.


Kadhalika Mkuu wa Mkoa amemtaka Mkuu huyo wa Wilaya huyo kuweka maeneo ya kipaumbele ili mwisho wa siku akiondoka aache alama na kumtoa hofu kuwa hawezi kufanya kila kitu lakini lazima awe na eneo la kipaumbele inaweza kuwa upande wa elimu, mazingira, ulezi na masuala kama hayo.


Akizungumza mara baada kuapishwa Mkuu wa wilaya ya Magu Mhe. Jubilate Win Lauwo amemshukuru Mkuu wa Mkoa kwa nasaha zake za uongozi na kuahidi kufanya kazi kwa bidii kwa kile alichokisema kuwa kazi ni ibada.


Mkuu huyo wa Wilaya ya Magu ameapishwa leo kufuatia uteuzi wa Mhe. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania alioufanya terehe 23 Juni, 2025 na ameteuliwa kufuatia utenguzi wa aliyekuwa Mkuu wa Wilaya hiyo.


Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • RC MTANDA AAGIZA USIMAMIZI THABITI WA VITUO VYA AFYA KUONGEZA MAPATO

    June 30, 2025
  • RC MTANDA AYASHUKURU MAKUNDI MBALIMBALI USHIRIKI ZIARA YA RAIS DKT. SAMIA

    June 30, 2025
  • RC MTANDA ATOA SOMO LA UONGOZI KWA DC MPYA MAGU

    June 30, 2025
  • KAMA TUNAHITAJI KUSONGA MBELE NI LAZIMA KUJIUNGA NA USHIRIKA – RAS BALANDYA

    June 24, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.