• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

RC MTANDA AVIAGIZA VYUO VIKUU, KATI KUSAJILI WANAFUNZI FAO LA MATIBABU NHIF

Posted on: November 10th, 2025

Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Said Mtanda amewataka wakuu wa vyuo mkoani humo kutoa elimu kwa wanafunzi wapya wanaodahiliwa pamoja na kuweka usimamizi mzuri wa kuhakikisha wanajiunga na fao la matibabu kutoka Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF).

Mhe. Mtanda ametoa agizo hilo mapema leo jumatatu tarehe 10 Novemba, 2025 wakati akifungua kikao kazi kilichoitishwa na NHIF kwa wakuu vyuo 42 vya mkoani humo chenye lengo la kupitia hali ya utekelezaji wa usajiri wa wanafunzi kwenye mfuko huo kwa ajili ya kuleta utulivu wa kimatibabu kwenye vyuo vyao.

“Twendeni tukafanikishe kila mwanafunzi anakua ndani ya mfuko huu kwani tukikusanya kwa pamoja ndipo tutaweza kutoa huduma bora lakini tukikusanya kwa uchache mfuko utashindwa kujiendesha vema kwani wachache watasajiriwa na wakiugua wote kwa wakati mmoja italeta utegemezi.” Mhe. Mtanda.

Aidha, amebainisha kuwa jukumu la utekelezaji wa mfuko wa bima ya afya kwa wote ni la kila mmoja hivyo kila chuo kisimamie kwa makini adhma hiyo ili kujihakikishia wanafunzi na jamii kwa ujumla inakua na uhakika wa matibabu mara tu wanapougua.

Aidha, amewaagiza mfuko huo wahakikishe wanaboreaha mifumo ya usajiri pamoja na kushirikiana na serikali hususani Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa (NIDA) kuondoa kwa haraka changamoto zinazochelewesha ukamilifu wa wanafunzi kwenye fao hilo.

Vilevile, ameviagiza vyuo kuwasilisha utekelezaji wa matakwa ya sheria ya bima ya afya kwa wote kwa kuhakikisha wawawasajili wanafunzi wote wanaostahili na kuwasilisha taarifa ya kila robo katika NHIF na Ofisi ya Mkuu wa Mkoa kwa ufuatiliaji.

Awali, Meneja wa Mfuko wa Bima ya Afya Mkoa wa Mwanza Ndugu Jarlath Nushashu alibainisha kuwa malengo ya kukutana na kundi hilo ni kupanga na namna ya kuimarisha na kuboresha usajiri wa wanafunzi wapya katika fao la wanafunzi ambalo lilianzishwa mwaka 2009 lililolenga kuwanufaisha wanafunzi kwa Tshs. 50,400 tu kwa mwaka.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • RC MTANDA AIPONGEZA OFISI YA WAZIRI MKUU KUANZISHA KAMATI ZA MAAFA ZA MIKOA

    November 18, 2025
  • RC MTANDA AWATAKA WATAKWIMU KUTOA TAKWIMU SAHIHI KUCHAGIZA MAENDELEO

    November 18, 2025
  • RAS MWANZA AONGOZA WAOMBOLEZAJI MAZISHI YA ALIYEKUWA MTUMISHI WA MWAUWASA

    November 14, 2025
  • MWANZA YASHIRIKI MAFUNZO KUKUZA USAWA WA KIJINSIA NCHINI MKOANI MOROGORO

    November 13, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.