• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

RC MTANDA AWAONGOZA WAOMBOLEZAJI MAZIKO YA BABA WA MKUU WA IDARA YA BIASHARA NA UWEKEZAJI

Posted on: November 7th, 2025

Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Said Mtanda leo Novemba 7, 2025 amewaongoza wafiwa,waombolezaji na watumishi katika mazishi ya aliyekuwa Baba mzazi wa Mkuu wa idara ya biashara, viwanda na uwekezaji katika Sekretarieti ya Mkoa Mzee Charles Karoli (92) katika makaburi ya familia Majengo - Ilula wilayani Magu.

Katibu Tawala Mkoa wa Mwanza Bw. Balandya Elikana ametoa salamu za pole kwa familia ya marehemu na amesema kwamba watumishi wote wa ofisi ya Mkuu wa Mkoa wanaungana na familia kwa kipindi hiki cha majonzi kwani wanajivunia upendo alionao Patrick kwa wenzake na ametoa rai kwa wana familia kumtegema mungu wakati wote hususani katika kipindi hiki kigumu.

Akiongoza ibada ya mazishi iliyofanyika katika kanisa Katoriki la Mt. Klaveri mjini Magu, Padri George Nzungu amewasihi waombolezaji kutengeneza mahusiano mema na Mwenyezi mungu kwa kufanya matendo mazuri ikiwa ni pamoja na kuwa na upendo baina yao huku akisisitiza kuwa upendo wa kweli huanzia katika familia zao hadi katika jamii.

Akimuelezea Marehemu, Padri Nzungu amesema marehemu Mzee Karoli aliishi maisha ya upendo na ukarimu kwa jamii iliyomzunguka na akahusianisha umati wa maelfu ya waombolezaji walioshiriki shughuli za mazishi hayo kuwa ni kutokana na mbegu ya kujali ambayo aliipanda mioyoni mwa watu enzi za uhai ambapo anatoa wito kwa jamii kumuenzi kwa matendo hayo mema.

Akitoa shukurani kwa niaba ya familia ya Mzee Karoli Mkuu wa idara ya biashara, viwanda na uwekezaji Bw. Patrick Karangwa amewashukuru waomboolezaji ikiwa ni pamoja na watumishi wenzake kwa kuonesha upendo wa kushiriki na kumsindikiza Baba yake mzazi katika safari yake ya milele.

Mzee Karoli alikua anasumbuliwa na maradhi ya saratani ya utumbo mkubwa na kwamba alipatiwa matibabu katika hospitali za BMC, KCMC,SHREE HINDU MANDAL, RABININSIA pamoja na Hospitali ya taifa Muhimbili ambapo umauti ulimfika Novemba 2, 2025.

Bwana ametoa, bwana ametwaa, jina lake lihimidiwe. apumzike kwa amani. Amina.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • RC MTANDA AIPONGEZA OFISI YA WAZIRI MKUU KUANZISHA KAMATI ZA MAAFA ZA MIKOA

    November 18, 2025
  • RC MTANDA AWATAKA WATAKWIMU KUTOA TAKWIMU SAHIHI KUCHAGIZA MAENDELEO

    November 18, 2025
  • RAS MWANZA AONGOZA WAOMBOLEZAJI MAZISHI YA ALIYEKUWA MTUMISHI WA MWAUWASA

    November 14, 2025
  • MWANZA YASHIRIKI MAFUNZO KUKUZA USAWA WA KIJINSIA NCHINI MKOANI MOROGORO

    November 13, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.