• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

RC MTANDA AWATAKA WATAALAMU SEKTA YA ARDHI KUWA WAADILIFU

Posted on: February 14th, 2025

RC MTANDA AWATAKA WATAALAMU SEKTA YA ARDHI KUWA WAADILIFU


Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Said Mtanda amewakumbusha wataalam wa Sekta ya Ardhi Mkoa wa Mwanza kuepuka vishawishi vya rushwa, kufuata kanuni, taratibu na sheria za ardhi, na kuhakikisha kila kero au mgogoro wa ardhi unafanyiwa kazi na kufika mwisho ili kujenga imani kwa jamii na Wananchi kuhusu utendaji wa sekta ya ardhi.

Mhe. Mtanda ametoa kauli hiyo mapema leo alipokuwa akifungua kikao kazi cha wataalamu wa sekta hiyo Mkoani Mwanza, Mhe. Mtanda amesema kwa sasa wananchi wengi hawana imani ya utendajikazi na sekta hiyo hivyo wanapaswa kutenda haki na kufanya kazi kwa weledi wa juu.

Mkuu wa Mkoa amesema katika malalamiko ambayo huwa anasikiliza na kutatua kila siku ya Jumanne asilimia themanini ya malalamiko hayo ni ya sekta ya ardhi, hivyo amewataka kuona ukubwa wa tatizo na kulishughulikia ipaswavyo.

“Nimeongea hivyo ili muone ukubwa wa tatizo na changamoto hii imesababishwa kwa asilimia kubwa na wataalam wa ardhi wenyewe kwa kutotimiza majukumu yao”. Amesema Mhe. Mtanda.

Sambamba na hayo Mkuu wa Mkoa amesisitiza juu ya umuhimu wa kuandaa maandiko pamoja na kuzishirikisha taasisi na mashirika yasiyoya kiserikali, kuwashirikisha wananchi pamoja na kutumia teknolojia rahisi na za kisasa katika upangaji wa miji ili kuharakisha maendeleo yawananchi.

Aidha Mkuu wa Mkoa amemshukuru na kumpongeza kwa dhati Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassani kwa mwaka wa fedha 2022/2023 kutoa kiasi cha Shilingi Bilioni 50, na kuipatia Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi ili zitumike kutekeleza mradi wa kupanga, kupima na kumilikisha maeneo nchini.

“Fedha hizo zilipelekwa kwenye Halmashauri 57 ikiwemo Halmashauri za Mkoa wa Mwanza ambazo ni Jiji la Mwanza (Milioni 800), Ilemela (Bilioni3.5) na Buchosa (Milioni 300), Sengerema (Milioni 200) na vyuo vitatu…”.

Naye Bi. Happyness Mtutwa Kamishna wa Ardhi Msaidizi wa Mkoa wa Mwanza amemshukuru Mkuu wa Mkoa kwa kutoa elimu nzuri na ushauri uliolenga kuboresha na kuimarisha sekta ya ardhi Mkoani Mwanza na kuahidi kiwa yale yote aliyoyasema Mhe. Mkuu wa Mkoa yatatekelezwa kwa kiwango cha juu na kwa wakati.


Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • MWANZA, SIMIYU ZANG'ARA UTAMILIFU DARASA LA SABA KANDA YA ZIWA

    May 30, 2025
  • RAS MWANZA AZINDUA RASMI MRADI WA KUPAMBANA NA UGONJWA WA SELI MUNDU

    May 30, 2025
  • WAANDISHI WA HABARI MWANZA WAPIGWA MSASA MIKAKATI YA KUTOKOMEZA WATOTO WA MITAANI

    May 29, 2025
  • RAS MWANZA AWATAKA VIONGOZI WA UMMA KUDUMISHA NIDHAMU NA UFANISI KAZINI

    May 26, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.