• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

RC MTANDA AWEKA JIWE LA MSINGI SHULE YA MSINGI YA AMALI KISHIRI, ATAKA IKAMILIKE NDANI YA WIKI TATU

Posted on: February 12th, 2026

Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Said Mtanda leo Februari 12, 2026 ameweka jiwe la msingi katika mradi wa ujenzi wa Shule Mpya ya Msingi ya Amali iliyopo Kata ya Kishiri, Jijini Mwanza, huku akitoa maagizo kwa Halmashauri ya Jiji la Mwanza kuhakikisha mradi huo unakamilika ndani ya muda wa wiki tatu kama ilivyopangwa.

Akizungumza baada ya kukagua maendeleo ya ujenzi huo, Mhe. Mtanda amesisitiza umuhimu wa kukamilika kwa mradi huo kwa wakati ili kuwezesha wanafunzi kuanza masomo katika mazingira bora na rafiki kwa maendeleo yao ya kitaaluma na kijamii.

“Naiagiza Halmashauri kuhakikisha muda waliopewa wanautumia vyema. Shule hii inapaswa kuanza kufanya kazi rasmi mara tu baada ya kukamilika. Hatuna sababu ya kuchelewa,” amesisitiza RC Mtanda.

Katika hafla hiyo, Mkuu wa Mkoa ametumia fursa hiyo pia kutoa pongezi za dhati kwa wazazi, walimu na wanafunzi wa Shule ya Sekondari Igoma kwa kufanya vizuri katika matokeo ya Mtihani wa Kidato cha Nne mwaka 2025, ambapo shule hiyo imeongoza kiwilaya katika Wilaya ya Nyamagana.

“Shule ya Sekondari Igoma imekuwa kinara wa ufaulu kwa Wilaya ya Nyamagana. Nawapongeza sana kwa matokeo mazuri. Endeleeni kuchapa kazi kwa bidii ili matokeo yawe bora zaidi mwaka hadi mwaka,” amesema.

Kwa upande wake, akisoma taarifa ya mradi kwa niaba ya Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Jiji la Mwanza, Mwalimu Mkuu wa Shule ya Sekondari Igoma, Anthony Masanja, amesema kuwa shule hiyo ilipokea kiasi cha Shilingi 330,700,000 mwezi Julai 1, 2025 kupitia Mradi wa BOOST kwa ajili ya ujenzi wa Shule Mpya ya Msingi ya Amali.

Ameeleza kuwa mradi huo unasimamiwa na Ofisi ya Mhandisi wa Jiji la Mwanza, huku mkandarasi anayetekeleza ujenzi huo akiwa ni Ndugu Eliawony Makundi.

Kwa mujibu wa taarifa hiyo, hadi sasa mradi umetekelezwa kwa asilimia 75, ambapo jumla ya Shilingi 258,600,000 tayari zimetumika. Kiasi kilichosalia ni Shilingi 72,100,000 kwa ajili ya kukamilisha kazi zilizobaki.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • MKURUGENZI IDARA YA MAAFA OWM AFUNGA MAFUNZO YA KUKABILIANA NA DHARULA MWANZA

    February 20, 2026
  • KAYA 19,344 KUNUFAIKA NA BIMA YA AFYA KWA WOTE MWANZA AWAMU YA KWANZA

    February 20, 2026
  • RC MTANDA AMPOKEA WAZIRI DEUS SANGU MWANZA

    February 20, 2026
  • RC MTANDA AWATAKA WASIMBE NA WABANZA KUUNGANA KUKATA BIMA YA AFYA KWA WOTE

    February 20, 2026
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.