• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

RC MTANDA AZIHIMIZA HALMASHAURI KUONGEZA KASI UKUSANYAJI MAPATO

Posted on: June 7th, 2024

RC MTANDA AZIHIMIZA HALMASHAURI KUONGEZA KASI UKUSANYAJI MAPATO


Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Said Mtanda amezitaka Halmashauri zote mkoani humo kuhakikisha wanafanya kazi ya usimamizi wa ukusanyaji wa mapato ya ndani ili kuzisaidia Halmashauri zao ziweze kujiendesha na kuepukana na hali ya ukata.

Mhe. Mtanda ametoa wito huo wakati akiongea na watumishi kwenye kikao kilichofanyika katika ukumbi wa Halmashauri ya Misungwi leo tarehe 07 juni, 2024.

Sambamba na ukusanyaji mapato Mhe. Mtanda pia amewataka Watumishi wa Umma kuzipenda kazi zao kwa kuendelea kufanya kazi kwa bidii huku wakizingatia utoaji wa haki kwa wananchi wanaostahili.

"Kazi ndio msingi wa utu, tuzipende kazi zetu, wapo wanaochezea kazi zao kwa kuamua hata kulewa pombe lakini mimi naamini kwenye kazi kupata kipato na kujenga heshima." Mhe. Mtanda.

Aidha, amewataka watumishi wote kusimamia miradi ya maendeleo ili ikamilike kwa wakati na daima wawe wakweli kwenye utendaji wao  kwani hali hiyo itasaidia kuleta mshikamano utaoimarisha maelewano kazini.

"Mtumishi yeyote wa umma anayetoa huduma bora kwanza atapendwa na viongozi wake lakini pia atapendwa na wananchi, pokeeni wateja kwa utayari kwa kuwasikiliza." Amesema Mkuu wa Mkoa wakati akisisitiza suala la utoaji huduma bora.

Vilevile, amewataka watumishi kwenye idara zao kuhakikisha wanakua na mipango ya muda mfupi na mrefu na kuhakikisha wanaifuata na kuikamilisha ili kuhakikisha wanatoa huduma bora kwa wananchi.

"Kufuata maadili ndio msingi mzuri wa kazi, tuwahi kazini na kuhakikisha tutekeleza majukumu yetu tena kwa wakati na sio kuwahi kazini na kushinda tunachezea simu hapana hiyo haikubaliki na tutachelewesha maendeleo kwa wananchi." Mkuu wa Mkoa.

Halikadhalika, ameipongeza halmashauri hiyo kwa kutekeleza vema maagizo ya viongozi kwa kusimamia ukusanyaji wa mapato hadi kukaribia kukusanya shilingi bilioni 4 tofauti na siku za nyuma ambapo walikua wanakusanya shilingi bilioni 2 pekee.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.