• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

RC MTANDA AZINDUA UGAWAJI BODABODA 100 KWA VIJANA WA ILEMELA

Posted on: December 22nd, 2025

Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Said Mtanda leo tarehe 22 Desemba, 2025 amezindua rasmi ugawaji wa pikipiki kwa vijana wa Ilemela chini ya ufadhili wa Mhe. Mbunge wa jimbo hilo ikiwa ni utekelezaji wa ahadi aliyoitoa wakati wa kuomba ridhaa ya kuliongoza jimbo hilo.

Akizungumza na wananchi katika tamasha lililofanyika katika viwanja vya Furahisha Mhe. Mtanda amewataka vijana walionufaika na mkopo huo kuwa waadilifu na waaminufu na kuhakikisha wanadumisha amani ya nchi wakiwa katika shughuli zao za kujikwamua kiuchumi na sio kuvunja amani ambayo ni tunu ya taifa.

Amesema kuwa serikali mkoani Mwanza imedhamiria kuwainua vijana kiuchumi na kwamba imeanzisha kanzidata ya kuwatambua na kuweka mikakati ya kuwaendeleza katika stadi za maisha pale itakapobidi ili mwisho wa siku wawe na nyenzo, mtaji na vifaa vya kujitafutia.

Aidha, amempongeza Mhe. Mbunge kwa kutimiza ahadi kwa wananchi wa Ilemela kupitia mpango kazi aliojiwekea wa kuhakikisha anawapatia mitaji ya kujiimarisha kiuchumi hususani kundi kubwa la vijana ambalo ameanza nalo.

“Serikali ina mipango thabiti ya kuwainua vijana kiuchumi ikiwemo kuanzishwa kwa wizara maalumu ya kushughulikia vijana sio kwa sera pekee bali kwa kuwawezesha moja kwa moja vijana ili waweze kupiga hatua kiuchumi.” Mhe. Mtanda.

Mbunge wa Jimbo la Ilemela Mhe. Kafiti Kafiti amesema tamasha linalochagizwa na ugawaji pikipiki 100 ni katika kutimiza ahadi yake ya kuwakwamua kiuchumi walemavu, vijana na wanawake katika maeneo ya Mitaji ya kuweza kujiajiri.

“Utakuta Bodaboda anapewa pikipiki ya Milioni tatu na anatakiwa arejeshe milioni sita, gharama za leseni zimekuwa kubwa na ninaahidi kuwasemea ili ipungue kutoka elfu 70 hadi 30 na katika eneo la Mafunzo nataka kuwashika mkono kupitia VETA zetu.” Amefafanua.

Vilevile, amebainisha kuwa vijana hao kwa sasa watatoa Tshs. 10,000 pakee kupata mafunzo VETA badala ya 100,000 na amewawekea dhamana benki na kwamba kila baada ya miezi 6 atawapatia pikipiki 100 na kwamba watarejesha Tshs. 2,000 pekee kwa siku kama marejesho.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • MRADI WA UMWAGILIAJI IBANDA–IGAKA WA BILIONI 35 HAUTASIMAMA – SILINDE

    January 10, 2026
  • RC MTANDA MGENI RASMI MECHI YA KIRAFIKI SIMBA VS PAMBA MWANZA

    January 10, 2026
  • BODI YA BARABARA MWANZA YATAKIWA KUSIMAMIA UBORA NA MATUMIZI SAHIHI YA FEDHA

    January 08, 2026
  • MHE. KUNDO KUKAGUA MIRADI YA MAJI MWANZA KWA SIKU TATU

    January 07, 2026
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.