• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

RC MTANDA AZITAKA KAMATI ZA USHAURI WA KISHERIA KATIKA MKOA WA MWANZA KUMALIZA NA KUTATUA MIGOGORO YA WANANCHI

Posted on: December 2nd, 2025

Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Said Mtanda ameziagiza Kamati za Ushauri wa kisheria Mkoa na Wilaya kuhakikisha wanasaidia wananchi kumaliza kero na changamoto zao na hatimaye kuondoa migogoro kwenye jamii.

Ametoa rai hiyo mapema leo tarehe 02 Disemba 2025 wakati akifungua kikao kazi cha viongozi wa Kamati ya Ushauri wa Kisheria Mkoa waliokutana na kamati za wilaya za mkoa huo katika ukumbi wa Bodi ya Pamba jijini Mwanza.

Mhe. Mtanda amesema ameanzisha na kuzindua Kamati ya Mkoa na za Wilaya ili kuona wananchi na wadau wengi wanapata elimu katika masuala mbalimbali ya kisheria na kutatua migogoro iliyopo kwenye jamii kwa mujibu wa sheria, kanuni na taratibu.

Aidha, ameipongeza Kamati ya Ushauri wa kisheria ya mkoa huo na kamati za wilaya kwa kuwa vinara wa kushauri wananchi, watumishi, taasisi na viongozi wa umma kuhusu masuala ya kisheria na akatoa wito makundi yote kuiona ili kupata ushauri na msaada kwa wakati.

Halikadhalika, ameziagiza ofisi za wakuu wa wilaya kuhakikisha wanashirikiana na kamati za ushauri wa kisheria kwenye maeneo yao kwa kuwa na kliniki maalumu za muda fulani ndani ya mwezi au juma za kusikiliza wananchi na kuhakikisha wanawatatulia kero zao mathalani za ardhi , mirathi na ndoa ambayo imekithiri.

Awali, Mwenyekiti wa Kamati ya Ushauri wa Kisheria Mkoa Wakili Mwandamizi Kabyemela Lushagara alibainisha malengo ya kikao kazi hicho kuwa ni kujengeana uwezo na kuandaa mpango kazi mfupi wa miezi sita na mrefu kwa miaka mitano wa utekelezaji wa shughuliza huduma za kisheria.

Aidha, amebainisha kuwa Kamati hiyo imejiandaa kuwahudumia wananchi kutoka kwenye maeneo yao bila kusafiri kwenda mjini kwa kutumia teknolojia ya kisasa ya kutumia mtandao ambao watautambulisha siku za usoni.

“Wananchi wanapokuja kwetu kuleta changamoto wanapoteza muda, maono yetu ni kuweka mpango maalum wa kuwasikiliza na kuwatatulia kero kwa kutumia mtandao ili wasipoteze muda na kwa mpango wetu hadi kipindi cha miaka 2 tutakamilisha hilo.” Wakili Lushagara.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • RC MWANZA AKUTANA NA VIONGOZI & WACHUNGAJI WA AICT ASISITIZA AMANI NA MSHIKAMANO

    December 02, 2025
  • TUWE WABUNIFU KWENYE KAZI TUSISUBIRI KUELEKEZWA- RAS BALANDYA

    December 02, 2025
  • RC MTANDA AZITAKA KAMATI ZA USHAURI WA KISHERIA KATIKA MKOA WA MWANZA KUMALIZA NA KUTATUA MIGOGORO YA WANANCHI

    December 02, 2025
  • RAS MWANZA AWAASA WAHITIMU KUTUMIA UBUNIFU, RASILIMALI KUTENGENEZA FURSA

    November 28, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.