• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

RC MTANDA, WAZIRI KAKURWA WAJADILI UFUGAJI NA UVUVI MWANZA

Posted on: December 26th, 2025

Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Said Mtanda, amefanya mazungumzo na Waziri wa Mifugo na Uvuvi Dkt. Bashiru Ally Kakurwa (Mb) ofisini kwake, yakilenga kuimarisha sekta za mifugo na uvuvi mkoani humo.

Mhe. Mtanda ameeleza changamoto ya upungufu wa chakula cha samaki licha ya kuongezeka kwa ufugaji wa samaki kwa vizimba, akiomba kuanzishwa kwa kiwanda cha chakula cha samaki.

Pia amebainisha fursa kubwa za uwekezaji katika eneo hilo, pamoja na umuhimu wa kuangalia upya shamba la mifugo la Mabuki ili kuvutia wawekezaji na kuongeza uzalishaji.

Ameongeza kuwa uboreshaji wa Uwanja wa Ndege wa Mwanza kuwa wa kimataifa utarahisisha usafirishaji wa nyama na samaki ndani na nje ya nchi, huku akiomba wizara kusaidia kutatua changamoto za tozo nyingi kwa viwanda vya samaki.

Kwa upande wake, Waziri Kakurwa amesema wizara imepokea maoni hayo na itayafanyia kazi, akisisitiza kuwa ziara yake ya kikazi katika wilaya za Nyamagana, Ilemela, Sengerema na Ukerewe inalenga kusikiliza wadau na wananchi.

Ameahidi kushughulikia suala la Mabuki, kuimarisha usafirishaji pamoja na kuanzisha mamlaka na bodi ya kusimamia masuala ya mifugo.

Waziri pia amepongeza hatua zilizopigwa katika ufugaji wa samaki kwa vizimba na matumizi ya asilimia 10 ya mapato katika Wilaya ya Nyamagana akisisitiza kuongeza boti za doria na kuhimiza halmashauri zote zinazopakana na Ziwa Victoria kuhamasisha ufugaji wa samaki kwa njia hiyo.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • MRADI WA UMWAGILIAJI IBANDA–IGAKA WA BILIONI 35 HAUTASIMAMA – SILINDE

    January 10, 2026
  • RC MTANDA MGENI RASMI MECHI YA KIRAFIKI SIMBA VS PAMBA MWANZA

    January 10, 2026
  • BODI YA BARABARA MWANZA YATAKIWA KUSIMAMIA UBORA NA MATUMIZI SAHIHI YA FEDHA

    January 08, 2026
  • MHE. KUNDO KUKAGUA MIRADI YA MAJI MWANZA KWA SIKU TATU

    January 07, 2026
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.