• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

RC Mwanza aagiza Halmashauri Sengerema kujenga Miundombinu ya Afya kila Kijiji

Posted on: June 24th, 2022


Mhandisi Robert Gabriel, Mkuu wa Mkoa wa Mwanza amewaagiza Halmashauri ya Wilaya ya Sengerema kuhakikisha wanajenga Miundombinu ya Afya kwenye kila Kijiji ili kusogeza huduma za afya kwa wananchi.

Mhe Mkuu wa Mkoa ametoa agizo hilo mapema leo ijumaa baada ya kuibuka hoja ya 2019/20 ya Upungufu wa Miundombinu ya Sekta ya Afya kwa kukosa Zahanati kwenye Vijiji 16 wakati Baraza la Madiwani la Halamshauri hiyo lilipokutana kujadili Hoja za Mdhibiti na Mkaguzi wa Hesabu za Serikali.


Mhe Mkuu wa Mkoa ametoa rai kwa Halmashauri hiyo kutenga fedha kwa ajili ya Ujenzi wa Miundombinu ili kupunguza pengo lililopo na jamii ihamasishwe kuchangia maendeleo ya miradi ya afya ili kupata rasilimali zaidi.

"Naomba ubunifu uwepo ili tupate Zahanati kwenye kila kijiji, tukikubaliana kwenye  kamati zetu tutafanikiwa na kule kijijini Mhe Diwani akitafuta mchanga na mawe kutoka kwa wananchi wake halafu Mkurugenzi akapeleka Saruji basi tutasogea hatutabaki hapa tulipo."


Aidha, ametoa rai kwa TAKUKURU kufuatilia utekelezaji wa miradi katika hatua za awali ili kuzuia upotevu wa fedha badala ya kusubiri mambo yaharibike na kupitia hilo amemuagiza Mkurugenzi kuhakikisha taratibu za kisheria zinafuatwa kwenye matumizi ya fedha.


"Lengo letu ni kuzuia hoja hivyo ni lazima tujifunze kufuata kanuni na taratibu za fedha na ninaona dalili zote za Halmashauri hii kuondokana na hoja zinazoepukika hivyo wataalamu naomba tushirikiane na waheshimiwa madiwani na kuwe na uwazi kwenye kila jambo." Mkuu wa Mkoa.

Vilevile, Katibu Tawala wa Mkoa Ngusa Samike amewaasa waheshimiwa Madiwani kutumia Hekima na busara katika kazi na kuongeza ushirikiano na wataalamu ambao wengi wao ni wageni kwenye Halmashauri hiyo ambapo amebainisha kuwa Halmashauri hiyo ipo kwenye marekebisho makubwa ya ufanisi ili kuwaletea maendeleo wananchi.


Kaimu Mdhibiti na Mkaguzi wa Hesabu za Serikali Mkoa wa Mwanza, Waziri Shabani amesema Mwaka 2020/21 Halmashauri ya Wilaya ya Sengerema ilikaguliwa na kupata Hati yenye Shaka.



Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.