• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

RC Mwanza ahamasisha Ujenzi wa Zahati 74 Kwimba

Posted on: June 17th, 2021

Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Mhandisi Robert Gabriel Luhumbi ameagiza ujenzi wa zahanati kwa vijiji  74  vilivyopo wilayani Kwimba,mkoani Mwanza visivyokuwa na huduma hiyo zijengwe ili wananchi wapate huduma kwa kila Kijiji.

Hayo ameyabainisha leo mara baada ya kupitia hoja za mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa hesabu za serikali (CAG) kwa mwaka 2019 hadi 2020,ambapo amewaagiza maofisa tarafa kwenye maeneo yao waitishe kikao na watendaji wa kata na vijiji ili kila Kijiji kipate ramani na wajilidhishe na eneo ili zoezi la ujenzi wa msingi wa zahanati kwa kila Kijiji uanze.

"Naomba muyabebe haya maagizo kwa sababu nyie ndio mnaomsaidia Mkuu wa Wilaya kwenye kata zenu ,tutafute mchanga na mawe na mimi nitakuja kuzunguka kata zote tunataka mwaka 2025 wakati Katibu wetu wa chama anasimama kwenye jukwaa anawanadi madiwani awe anasema tuliahidi tunatekeleza," amesema na kuongeza

"74 ni idadi kubwa  mno huko nilipotoka kazi imeanza maboma yanakwenda kwa hatua mbalimbali,nimetoka Buchosa wanaupungufu wa zahanati  24, Sengerema 30 hapa 70 vijiji vyote hivyo wananchi wanahitaji huduma nitakuja kwenye kata na tarafa zenu zote Mwenge wa uhuru ukiondoka mimi naingia saiti tutakutana ili tujue kazi inaendeleaje tulishafanya majaribio hayo ikakubali na hapa itakubali,"alieleza Mhandisi Luhumbi.


Pia amesema,andiko la mradi liandikwe kwa kiswahili na wasimfiche mtu kwa lugha ya kiingereza ili ashindwe kuelewa,lengo ni kuboresha wapo kwenye mapambano ya kuleta maendeleo.


Aidha amewataka  wataalamu kuonesha  thamani ya fedha na wataenda  kukagua majengo kama wamepigwa ama  hawajapigwa kwa sababu wanajua hiyo inatokana uzoefu,endapo kunamtu  mzembe asiyefanya kazi wamuweke pembeni kwani  maendeleo lazima  yaende mbele .

Amesema kikubwa ni utekelezaji wa maelekezo yaliyotolewa,wanahitaji kufanya mapinduzi katika usimamizi wa miradi,amepitia hizo hoja lazima awe muwazi kwa hoja mpya 2019/ 2020 wamefanya vizuri.

"Millioni 80 nimejenga shule ambapo kwenye BOQ ni vyumba vinne mimi nilijenga shule mpya ya msingi yenye vyumba vya  madarasa saba na ofisi mbili lazima tutumie vizuri fedha ya umma inayokuja,lazima tuwe na mawimbi ya maendeleo pia madiwani watafute ardhi ambayo wanaweza kuwekeza miradi ambayo 1wanaweza kupata mapato mazuri kama kuanzisha majengo  ya biashara ili kuchochea maendeleo,"alieleza.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. July 29, 2022
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2022 July 03, 2022
  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI ICAP October 21, 2022
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • RC Malima ataka adhabu kali na marekebisho ya Sheria za barabarani dhidi ya wanaosababisha ajali kwa uzembe

    March 17, 2023
  • Tupo katika mchakato wa Katiba mpya-Mhe.Dkt.Ndumbaro

    March 17, 2023
  • Miaka miwili ya Rais Samia madarakani,Mwanza yajivunia kasi ya miradi ya maendeleo

    March 15, 2023
  • Mufti wa Tanzania Sheikh Dkt.Abubakar Zuber akemea maovu ndani ya Jamii

    March 15, 2023
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 33180, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras.mwanza@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.