• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

REDIO ZA JAMII ZATAKIWA KUELIMISHA UMMA KUFAHAMU MFUMO WA M-MAMA

Posted on: November 8th, 2024

REDIO ZA JAMII ZATAKIWA KUELIMISHA UMMA KUFAHAMU MFUMO WA M-MAMA


Mganga Mkuu Mkoa wa Mwanza Dkt. Jesca Lebba ametoa wito kwa Redio za jamii kusaidia kuelimisha umma juu ya mfumo wa M-Mama unaotoa fursa ya usafiri wa dharula kwa Mama na Mtoto mchanga kuanzia kwenye ngazi ya jamii hadi kwenye vituo vya kutolea huduma wakati wa dharula.

Akifungua semina ya mafunzo kwa Redio za jamii kutoka mikoa ya kanda ya ziwa kwenye hoteli ya Gold Crest jijini Mwanza leo Novemba 08, 2024 Dkt. Lebba amesema wanahabari kutoka kwenye Redio za kijamii wana nafasi kubwa ya kusaidia wananchi kuweza kufahamu mfumo huo ulioletwa mahsusi kwa ajili ya kuokoa maisha.

Ameongeza kuwa katika tafiti zilizofanyika imeonekana kumekua na ucheleweshaji wa taarifa, miundombinu duni ya kufika kwenye vituo vya kutolea huduma pamoja na ucheleweshaji kwenye kupatiwa huduma mara wafikapo wagonjwa hospitali hivyo mfumo huo umekuja na suluhisho kwenye adha hizo.

"Ndugu washiriki, tangu kuanza kwa mfumo huu mpaka sasa zaidi ya dharula elfu 98 zimesafirishwa na kwa Mwanza pekee ni zaidi ya dharula elfu 6 kwa wastani wa 300 kwa mwezi zimefikiwa."

Amefafanua Dkt. Lebba.

Aidha, mganga huyo wa mkoa amezitaka halmashauri kuhakikisha magari ya wagonjwa (Ambulance) yanakua tayari kutoa huduma wakati wote pamoja na kulipa kwa wakati kwa madereva ngazi ya jamii kwa mujibu wa mkataba yaani ndani ya siku 14 tangu watoe huduma wawe amelipwa.

"Naamini redio zetu mtatusaidia sana kuelimisha jamii kuwa huduma hii inapatikana kuanzia ngazi ya jamii na kwenye vituo vya kutolea huduma, matumizi sahihi ya namba 115 kwa ajili ya kuwaokoa wajawazito pamoja na watoto wachanga." Amesema Mganga Mkuu.

Awali, Mratibu wa mfumo wa M-Mama kutoka Mkoa wa Mwanza Stanley Kajuna amesema kuwa walengwa waliokusudiwa zaidi ni mama mjamzito, mama aliyejigungua mpaja siku 42, mtoto mchanga hadi siku 28 na jamii kwa ujumla na kwamba tayari kuna madereva 4000 wamesajiriwa.

Katika kusaidia jamii, Mfumo wa M-Mama unachagizwa na kaulimbiu isemayo M- Mama Okoa maisha na inaendeshwa bila malipo yoyote kwa wateja kuanzia kwenye simu hadi usafiri wa kwenda kwenye kituo cha kupata huduma za afya.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.