• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

Serikali Yaahidi kuendelea kuboresha Mazingira ya kazi kwa Wauguzi nchini

Posted on: May 12th, 2023

**Serikali yaahidi kuendelea kuboresha mazingira ya Wauguzi nchini.*


Waziri wa Afya Mhe. Ummy Mwalimu ameahidi Serikali kuendelea kuboresha mazingira ya kazi kwa Wauguzi nchini kutokana na kutambua mchango wao katika Sekta ya afya nchini.

Akizungumza kwa niaba yake katika hafla ya ufungaji wa Mkutano Mkuu wa Chama cha Wauguzi nchini TANNA kwenye ukumbi wa Malaika Resort, Katibu Tawala wa Mkoa wa Mwanza, Ndg.Balandya Elikana amesema Serikali imekuwa ikiweka kipaumbele cha bajeti Sekta ya afya kwa kuboresha huduma zote kwa ujumla yakiwemo mazingira ya Wauguzi.

Amesema siyo rahisi kutatua changamoto zote kwa mara moja zinazowakabili kada hiyo,lakini kadiri bajeti inaporuhusu kipaumbele kitawekwa lengo likiwa kuboresha kwa ujumla Sekta ya afya nchini

"Nimesikia katika risala yenu baadhi ya changamoto zinazowakabili,yale ya ngazi ya Mkoa tutayafanyia kazi na yale yaliyo juu ya uwezo wetu yatafikishwa TAMISEMI ili yapatiwe ufumbuzi",amesema Mtendaji huyo wa Mkoa

Aidha amewakumbusha Wauguzi hao Mkutano huo wa siku tano uliofanyika Mwanza umeambatana na makongamano mbalimbali ya Kisayansi,wayatumie kama chachu ya kuongeza ufanisi wa kazi watakaporudi makazini.

"Kipaumbele chetu sasa ni ubora wa huduma,wakati Serikali ikizidi kuwekeza katika Sekta ya afya,Wauguzi nao wanaendelea kupatiwa mafunzo mbalimbali yakilenga staha,heshima na maadili ili wateja waendelee kupatiwa huduma bora,hadi sasa Wauguzi 2500 wamepatiwa mafunzo hayo",Saturin Mwanangwa,Mkurugenzi wa huduma na uuguzi Wizara ya Afya.

"Licha ya mazingira yenye changamoto kwa Kada hii ikiwemo kutoa huduma kwa wateja wengi,lakini tutaendelea kusimamia kiapo chetu cha kuwa watumishi wenye weledi,"Alexander Baluya,Rais wa TANNA.

Ufungaji huo umekwenda pamoja na Maadhimisho ya siku ya Wauguzi Duniani inayofanyika kila Mei 12 yaliyokwenda pamoja na kurudia kiapo kwa Wauguzi hao akikumbukwa mwanzilishi wa huduma za uuguzi na ukunga Duniani,Florence Nightingale raia kutoka Italia.

Mara baada ya kutoka katika ufungaji huo, Katibu Tawala wa Mkoa wa Mwanza Balandya Elikana amemtaka Mkandarasi aliyepewa kazi ya ujenzi wa Kituo cha Mawasiliano na Uokozi Ziwa Victoria chini ya Jumuiya ya Afrika Mashariki EAC kumaliza mradi huo kwa wakati na kuzingatia ubora na thamani kutokana na majanga ya ajali yanayotokea mara kwa mara Ziwani humo.

Mkandarasi Obuntu kutoka Uganda anatarajiwa kukamilisha ujenzi huo ndani ya mwaka mmoja.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.