• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

UJENZI WA MADARASA YA GHOROFA UBUNIFU MATUMIZI BORA YA ARDHI

Posted on: July 28th, 2025

Kutokana na ongezeko la watu na mahitaji ya ardhi kuwa makubwa katika maeneo mengi ya majiji nchini, Jiji la Mwanza limejipanga kufanya matumizi bora ya ardhi kwa kujenga madarasa kwa mfumo wa ghorofa ili kukidhi upatikanaji wa madarasa mengi katika eneo dogo.

Hayo yamebainika leo katika ziara ya ukaguzi wa miradi ya maendeleo aliyoifanya Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Said Mtanda katika shule ya msingi ya mchepuo wa kiingereza na kukuta ujenzi wa madarasa 11 kwa mfumo wa ghorofa yanayogharimu zaidi ya Milioni 665 ambao umesaidia kupata madarasa mengi kwa eneo dogo.


Akizungumza baada ya ukaguzi huo, Mhe. Mkuu wa Mkoa amewapongeza Jiji la Mwanza kwa ubunifu huo na kubainisha kuwa kwa kufanya hivyo wataweza kupata madarasa mengi kwenda juu na kufuta msongamano wa wanafunzi kwenye madarasa bila kuanzisha ujenzi wa shule mpya pembezoni.

Amesema, maendeleo ya teknolojia yanashabihiana na uamuzi huo kwani unaruhusu uwekaji wa mifumo yote muhimu katika miundombinu kwa gharama nafuu katika eneo dogo kwa kuwa na madarasa, maabara na matundu ya vyoo katika eneo moja.

Aidha, Mkuu wa Mkoa ameipongeza Sahule ya sekondari Nsumba kwa kufunga mfumo wa nishati asilia kwa ajili ya kupikia uliogharimu Tshs. Milioni 7.8 ambao amesema utasaidia kupunguza gharama za uendeshaji na kupunguza uchafuzi wa mazingira ukilinganisha na matumizi ya kuni ya siku za nyuma.


Pamoja na kuwapongeza kutokana na kufaulisha katika madaraja ya 1-3 kwa wanafunzi wote waliomaliza kidato cha sita 2025 shuleni hapo, Mhe. Mtanda amekagua ufugaji wa samaki kwa njia ya kisasa ya vizimba unaofanywa na vikundi vya vijana 4 katika Mwalo wa Luchelele waliokopeshwa Milioni 360 na halmashauri hiyo.

Sambamba na hayo Mkuu wa Mkoa ameshuhudia jinsi halmashauri ya jiji ilivyoamua kutenga Tshs. Milioni 150 kusaidia ujenzi wa kituo cha polisi cha Nyegezi kinachojengwa kwa Tshs. Milioni 232, Milioni 708  zilizojenga miundombinu ya Kituo cha Afya Mkolani pamoja na 300 zilizonunua vifaa tiba ili kuwasogezea huduma wananchi wa maeneo hayo.


Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • WAKULIMA WAASWA KUTUMIA TEKNOLOJIA KUFANYA KILIMO CHA KISASA

    August 02, 2025
  • RMO MWANZA AONGOZA ZIARA YA MAFUNZO YA USAFI NA MAZINGIRA MKOANI IRINGA

    July 21, 2025
  • RAS BALANDYA ATOA MAAGIZO UTEKELEZAJI WA MIRADI SENGEREMA

    July 30, 2025
  • UIMARISHWAJI WA MIFUMO YA KIELETRONIKI IMEONGEZA UWAJIBIKAJI – RAS BALANDYA

    July 23, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.