• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

Wadau Mwanza wawafuta machozi Wanafunzi waliounguliwa na Bweni Bwiru Sekondari

Posted on: June 30th, 2022



Kufuatia kuungua moto kwa bweni la wanafunzi wa kidato cha kwanza katika shule ya Sekondari ya Wavulana Bwiru iliyopo wilayani Ilemela jana usiku wadau mbalimbali wametoa Misaada kwa wanafunzi walioathirika ili kusaidia kurejesha maisha ya wanafunzi hao katika hali ya kawaida.

Akikabidhi vifaa hivyo kwa wanafunzi, leo Juni 30, 2022 Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Mhandisi Robert Gabriel amewashukuru Mhe Mbunge wa Ilemela, Bwana Peter, Desk and Chair foundation, CRDB, Nyakato Steel, NMB na wadau wengine mbalimbali walioguswa na maisha ya wanafunzi hao.


"Kwa niaba ya uongozi wa Mkoa wa Mwanza na zaidi timu ya Maafa nipende kutoa shukrani za dhati kwa wadau mbalimbali walioguswa na kuwasaidia watoto wetu waliopata majanga na hapa tunaona watoto wamepata mabati, magodoro, vyombo vya chakula, suruali, mashati, viatu, Chandarua, Masweta na mashuka." Mkuu wa Mkoa.

Aidha, Mkuu wa Mkoa amewaondoa hofu wazazi na wananchi kuwa watoto kwenye shule hiyo wapo salama na masomo yanaendelea kama kawaida kwani huduma zote zinaendelea kutolewa na wanafunzi hao wameshaanza kupata vifaa.

"Sisi kama wilaya ya Ilemela, tunakushukuru sana Mhe Mkuu wa Mkoa kwani usiku wa jana ulituahidi kuwa ndani ya saa 24 vifaa vilivyoteketea vitapatikana na kwa maelekezo uliyoyatoa tunakuahidi tutatumia siku tatu tu tunakamilisha ujenzi wa jengo la bweni lililo pale juu." Mhe. Salumu Kalli, Kaimu Mkuu wa wilaya ya Ilemela.

"Kwa niaba ya Benki ya NMB tunawapa pole wanafunzi wote kwa janga lililowapata, tuliposikia janga hili limetokea tumeamua kuja kuwapa pole na tumeambiwa kuwa kuna bweni linajengwa na lipo kiwango cha kuezeka nasi tumekuja na bati bando 11 zenye thamani ya Tshs Milioni 5." Meneja wa Kanda wa NMB, Baraka Ladslaus.

"Tatizo au janga hili lisiwavunje moyo, muwe na ujasiri na endeleeni kuwaombea waliowafadhili tena fanyeni jitihada kwenye masomo kwani kupata nafasi kwenye shule hii si kazi nyepesi hivyo nyie mna bahati sana. Amesema Alhadj Sibtain Meghjee, Mwenyekiti Mkaazi wa Desk and Chair foundation aliyetoa Msaada wa Magodoro, Vyandarua na shuka vilivyogharimu Tshs Milioni 3.4

Awali, Mkuu wa Shule hiyo Mwalimu Thomas Werema alisema moto umeteketeza vifaa vyote vilivyokuwemo kwenye bweni la wanafunzi majira ya saa 3 usiku wakati wanafunzi wakiwa darasani wanajisomea na waliopata majanga ni wanafunzi 76 lakini wote wapo salama hakuna aliyedhurika.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.