• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

WAKAZI 3147 KIJIJI CHA MHULYA KWIMBA WANUFAIKA NA MRADI WA MAJI

Posted on: September 14th, 2024

WAKAZI 3147 KIJIJI CHA MHULYA KWIMBA WANUFAIKA NA MRADI WA MAJI


Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Said Mtanda amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuongeza upatikanaji wa maji safi na salama kwa wananchi wa kijiji cha Mhulya kutoka 40% hadi 90% kutokana na kuwajengea mradi wa maji wenye thamani ya Tshs. 667.1 milioni fedha za mfuko wa maji wa Taifa na PforH.

Mhe. Mtanda ametoa shukrani hizo leo tarehe 14, 2024 katika Kijiji cha Mhulya kilichopo Kata ya Ngula Wilayani Kwimba wakati akikagua mradi wa maji kutoka kwenye chanzo cha kisima kirefu cha mita 80 chenye uwezo wa kuzalisha maji lita 12,336 kwa saa ambao umekamilika tangu mwezi juni 2023 chini ya usimamizi wa Wakala wa Maji na Usafi wa Mazingira Vijijini (RUWASA).

Aidha, Mhe. Mtanda amewataka wananchi kulinda miundombinu ya mradi huo na viongozi wanaosimamia jumuia ya watumia maji kuketi na wananchi na kukubaliana nao juu ya bei ya kuuziana maji kwenye mradi huo.

 "mnaweza mkaamua kama uchangiaji wa huduma na fedha zinazopatikana zitumike kufanya ukarabati na marekebisho ya miundombinu itakapohitajika". Ameongeza Mhe. Mtanda.


Vilevile, Mkuu wa Mkoa amewahamasisha wananchi hao kujiandikisha kwenye orodha ya daftari la wapiga kura na kushiriki katika uchaguzi wa serikali za mitaa utakaofanyika novemba 27.

Naye Meneja wa RUWASA Wilaya ya Kwimba Mhandisi Godliva Gwambasa amesema mkandarasi KPR ameshakamilisha kazi na maji yanatoka kwenye vituo vyote 9 vya kutolea maji kwenye kijiji hicho na mradi huo kwa sasa unaendeshwa na wananchi wenyewe chini ya chombo cha kuendeshea maji (CBWSO) cha kijijini hapo.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.