• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

WANANCHI BUCHOSA WAASWA KUJITOKEZA KUSHIRIKI UCHAGUZI MKUU

Posted on: August 31st, 2025

Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa Bwana Ismail Ali Ussi amewaasa wananchi kushiriki Uchaguzi Mkuu utakaofanyika Oktoba 29, 2025 kuwachagua Wabunge, Madiwani na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Ametoa wito huo leo Agosti 31, 2025 wakati akiongea na wananchi katika kijiji cha Bukokwa na maeneo ya jirani wakati akikagua utekelezaji wa ujenzi wa maduka 20 yanayojengwa kwa fedha za mapato ya ndani ya Halmashauri hiyo kwa lengo la kupata chanzo cha kudumu cha ukusanyaji mapato.

Bwana Ussi amewasisitiza wananchi hao kuhusu umuhimu wa kujitokeza kupiga kura na kuzingatia taratibu za kisheria siku ya uchaguzi ili kulinda amani ya nchi. 

Kadhalika amewataka vijana kutokutumiwa na wanasiasa wenye malengo ya kujinufaisha binafsi kwa kuanzisha vurugu, na badala yake amewataka kuwa mabalozi wa amani na mshikamano katika kipindi chote cha uchaguzi.

Aidha, amewasihi katika kuamua ni nani wa kumchagua wahakikishe wanachagua viongozi sahihi ambao wana kiu ya kuwaletea maendeleo kupitia atakayewapigiania kuwaletea huduma bora za kijamii kama maji safi na salama, elimu na pembejeo za kilimo.

Kadhalika, amewaalika kujitokeza kwa wingi katika uchaguzi huo ili kuleta maana ya Uchaguzi mkuu ukilinganisha na idadi ya wananchi waliojiandikisha na kuboresha taarifa zao katika daftari la kudumu la wapiga kura katika zoezi lililoendeshwa na Tume huru ya Uchaguzi.

Halmashauri ya Wilaya ya Buchosa ni Halmashauri ya nane (08) na ya mwisho kwa Mkoa wa Mwanza kukimbiza Mwenge wa Uhuru mwaka 2025 chini ya kaulimbiu isemayo ‘Jitokeze kushiriki Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2025 kwa Amani na Utulivu.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • RC MTANDA AKABIDHI MAGARI YA BILIONI 1.3 KWA JESHI LA POLISI

    September 12, 2025
  • SERIKALI KUENDELEA KUTATUA CHANGAMOTO ZA WATUMISHI NCHINI

    September 11, 2025
  • MAJALIWA AAGIZA KUIMARISHWA ZAIDI SEKTA YA UFUATILIAJI, TATHMINI NCHINI

    September 11, 2025
  • NSSF WAFANYA ZIARA YA UWEKEZAJI MWANZA

    September 10, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.