• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

WANANCHI WA KATA YA KISEKE - ILEMELA WAMSHUKURU RAIS SAMIA KWA KUJENGEWA SHULE YA SEKONDARI

Posted on: October 19th, 2023

WANANCHI WA KATA YA KISEKE - ILEMELA WAMSHUKURU RAIS SAMIA KWA KUJENGEWA SHULE YA SEKONDARI


*Zaidi ya Milioni 584 zatumika kujenga Miundombinu ya shule hiyo Mpya*


*Itasaidia kuondoa msongamano wa wanafunzi kwenye shule Mama ya Angelina Mabula*


*Kusaidia kuondoa adha ya kutembea umbali mrefu kufuata huduma ya elimu*


*RC Makalla aagiza kujengwa uzio kwenye shule hiyo*


Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. CPA Amos Makalla anaendelea na ziara yake ya usikilizaji na utatuzi wa kero za wananchi pamoja na ukaguzi wa miradi ya maendeleo na mapema leo asubuhi amekagua ujenzi wa shule mpya ya Sekondari inayojengwa kwenye kata ya Kiseke wilayani Ilemela.

Akizungumza kwa niaba ya wananchi Diwani wa Kata ya Kiseke Mhe. Ramadan Mwevi amemshukuru Rais Samia Suluhu Hassan kwa kuwaondolea wanafunzi adha ya kutembea umbali mrefu kufuata elimu kwenye shule mama ya Angelina Mabula kutokana na kutoa zaidi Milioni 584 kupitia mradi wa Sequip.

Mhe. Mwevi amesema kwa muda mrefu watoto wamekua wakisongamana kwenye shule ya Sekondari ya Angelina ambayo ndio shule mama lakini kwa usikivu wa Rais Samia ameamua kuwaondolea adha hiyo watoto ndipo akaleta fedha za kujenga shule hiyo mpya kabisa ambayo ipo katika hatua za mwisho kukamilika.


"Kwa niaba ya wananchi wa Kata ya Kiseke, ninamshukuru sana Mhe. Samia Suluhu Hassan Rais wetu kwa kutuletea fedha hizi kujenga shule ya Sekondari kwenye kata yetu maana tumeondokana na adha za msongamano darasani na umbali kwenda kwenye shule mama, lakini pia ujenzi huu umetoa ajira za muda kwa vijana wanaojenga na mama lishe." Mhe. Diwani.

Akizungumza kwenye ukaguzi huo, Mkuu wa Wilaya ya Ilemela Mhe. Hassan Masalla amebainisha furaha yake kwa kupata mradi huo kwa kuahidi kukamilisha ujenzi ifikapo Novemba 15, 2023 ili watoto waanze kupata elimu kwenye shule hiyo mapema shule zitakapofunguliwa mwakani.

Mhe. Mkuu wa Mkoa ametumia wasaa huo kumshukuru Rais Samia kwa kuboresha huduma za elimu na akawaahiza halmashauri kuhakikisha wanalinda Miundombinu hiyo na watoto kwa kujenga uzio kuzunguka shule hiyo ambapo amebainisha kuwa utasaidia kupunguza migogoro ya ardhi.


Akikagua ujenzi wa hospitali ya wilaya ya Ilemela kwa zaidi ya Bilioni 3.4 iliyopo kwenye kata ya Sangabuye Mhe. Makalla amewataka LATRA kwa kushirikiana na Jeshi la polisi kuweka utaratibu wa daladala kufika kwenye hospitali hiyo ili kuwapunguzia wananchi gharama za usafiri wa kufika kupata huduma.


Awali akikagua maendelezo ya ujenzi wa barabara ya Nyakato (VETA)-Buswelu hadi Muhonze (KM 2.5) kipande kinachojengwa kwa Bilioni 2.9 CPA Makalla amewataka TANROADS kusimamia ubora na wananchi kulinda Miundombinu hiyo hususani taa ambazo wananchi wamekua na mtindo wa kuziiba.

Mhe. Mkuu wa Mkoa amehitimisha ziara wilayani Ilemela kwa kushiriki zoezi la kulaza bomba ardhini kama ishara ya uboreshaji mfumo wa usambazaji maji ambao utawanufaisha wananchi wa Buswelu, Kahama, Nyamadoke, Busenga, Bulela A, Zembwela na Kangae umbali wa Kilomita 49.4 kwa Bilioni 4.7.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.