• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

WANANCHI WAASWA KUBADILI MTINDO WA MAISHA ILI KULINDA AFYA YA MOYO

Posted on: September 29th, 2025

“Wananchi wanapaswa kubadili mtindo wa maisha na kuzingatia lishe bora ili kuepuka magonjwa ya moyo,” amesema Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Mhe. Said Mtanda wakati wa Maadhimisho ya Siku ya Moyo Duniani yaliyofanyika leo Septemba 29, 2025 katika Uwanja wa Hospitali ya Kanda ya Rufaa ya Bugando, Jijini Mwanza.

Maadhimisho hayo yamelenga kuongeza uelewa kuhusu magonjwa ya moyo, ambayo yamekuwa chanzo kikuu cha vifo duniani, na yamehudhuriwa na wadau mbalimbali kutoka sekta ya afya, mashirika yasiyo ya kiserikali na wananchi wa kawaida.

Akizungumza mbele ya mamia ya wananchi waliohudhuria, Mkuu huyo wa Mkoa amesisitiza kuwa magonjwa yasiyo ya kuambukiza, ikiwemo maradhi ya moyo, yameendelea kuwa chanzo kikuu cha vifo nchini na duniani kote, hali inayohitaji hatua za haraka.

Kadhalika, Mkuu wa Mkoa amewataka wananchi kujenga tabia ya kupima afya mara kwa mara na kutambua hali ya moyo wao mapema kabla ya kuathirika zaidi.

“Tusiishi kwa mazoea ya kwenda hospitali tu pale tunapougua. Magonjwa ya moyo yanaweza kuzuilika iwapo tutajenga utamaduni wa kupima afya mara kwa mara na kuchukua hatua mapema,” amesema RC Mtanda.

Kwa upande wake, Mkurugenzi Mkuu wa Hospitali ya Rufaa ya Kanda Bugando (BMC) Sr. Dr. Alicia Massenga amesema 20% ya watoto wanaozaliwa katika Hospitali hiyo wanakuwa na changamoto ya moyo na nusu yao wanahitaji matibabu ya upasuaji hivyo kulazimika kupelekwa JKC.

Amesisitiza kuwa bado suala la uelewa liko chini na kupelekea kuleta wagonjwa wakiwa wamechelewa hivyo kupendekeza uwepo wa utoaji wa mafunzo endelevu na upimaji wa moyo katika vituo vya afya.

Naye, Mganga Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Dkt. Jesca Lebba amesema Mwanza kuna jumla ya vituo 565 vinavyotoa huduma ya afya ikiwemo Bugando na elimu mbalimbali kuhusu masuala ya Afya imekuwa ikitolewa ikiwemo Moyo, lishe, umuhimu wa mazoezi.

Kauli mbiu ya mwaka huu ni “Kila Pigo la Moyo ni Maisha, Lilinde Usilipoteze”.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • WAZEE ZINGATIENI LISHE BORA KUJIKINGA NA MARADHI - RC MTANDA

    September 29, 2025
  • WANANCHI WAASWA KUBADILI MTINDO WA MAISHA ILI KULINDA AFYA YA MOYO

    September 29, 2025
  • PROGRAMU YA WANAWAKE NA SAMIA SI YA KUBEZWA NI FURSA YA KUKUA KIUCHUMI - RC MTANDA

    September 27, 2025
  • RAS BALANDYA APOKEA UGENI KUTOKA WIZARA YA MADINI

    September 26, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.