• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

WANANCHI WANAOTAKIWA KUFIDIWA KUPISHA UWANJA WA NDEGE MWANZA WATAKIWA KUWA NA SUBIRA

Posted on: February 21st, 2025

WANANCHI WANAOTAKIWA KUFIDIWA KUPISHA UWANJA WA NDEGE MWANZA WATAKIWA KUWA NA SUBIRA


Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Said Mtanda amewasihi Wananchi wa mitaa mitano iliyoko katika Kata ya Shibula Wilaya ya Ilemela Mkoani Mwanza wanaokabiliwa na mgogoro wa mpaka wa uwanja wa ndege kuwa watulivu wakati serikali ikiendelea kutafuta suluhu.

Mhe. Mtanda ameyasema hayo leo Februari 21, 2025 alipokuwa akizungumza na Wananchi wa Mitaa hiyo katika mkutano wa hadhara uliofanyika Mtaa wa Nyamilolelwa na kuwataka kuendelea kuwa wastahimilivu wakati Serikali ikiendelea na uchakataji wa upatikanaji wa suluhu.

Mkuu wa Mkoa amefanya mkutano huo ikiwa ni mara baada ya Mbunge wa Jimbo la Ilemela kuuliza swali bungeni la ni lini serikali itawalipa fidia wakazi wa mitaa mitano ya kata ya Shibula ambapo majibu ya Waziri wa ardhi alisema kuwa wananchi hao wapewe viwanja mbadala kauli iliyozua utata na mkanganyiko baina ya wahanga hao.

Akuzungumza na Wanachi hao, Mkuu wa Mkoa amesema Serikali inaendelea na mchakato wa majadiliano ili waje na uamuzi sahihi ambapo kwa siku ya leo yeye pamoja na Kamati ya Usalama Mkoa wameamua kuja uwandani kwa lengo la kujionea eneo la mgogoro wawe na uelewa wa pamoja ili waweze kuishauri Wizara na Serikali kuhusu utatuzi wa mgogoro huo.

Mimi kama Mkuu nimeona ni lazima niende na kamati yangu ya usalama kutembelea uwandani, wote hapa tulikuwa hatujafika eneo la mgogoro na ninatambua tayari kuna tathmini kadhaa zimeshafanyika ikiwemo ile ya kwanza ya shilingi bilioni 19, tathmini ya pili ya bilioni 26 nimekuja kuwaomba endeleeni kuwa wastahimilivu. Ameongeza Mkuu wa Mkoa.

Aidha Mkuu wa Mkoa amesema kama Serikali ya Mkoa haijapokea taarifa kamili ya maandishi  kuhusu uamuzi wa kauli hiyo iliyotolewa na Waziri wa ardhi hivyo wataendelea kujadiliana na kusubiri tamko rasmi la kimaandishi.

“Tunaendelea kutafuta ufumbuzi wa jambo hili na kwa kuwa tayari tumeshakusanya maoni yenu, na maoni yenu yote matano mliyotupatia,  tupeni muda kama serikali ili tuweze kushauriana vizuri na tuje na muafaka”.

Mgogoro huo wa mipaka ya uwanja wa ndege Mkoa wa Mwanza umedumu kwa takribani miaka 8 sasa ambapo Mkuu wa Mkoa amesema yuko tayari kuhakikisha Serikali inaumaliza mgogoro huo kwa kuwa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ni sikivu na watafikia maamuzi ambayo ni sahihi.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.