• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

Watumishi wa Umma Mwanza wakumbushwa kutambua wajibu wao

Posted on: May 15th, 2023

*Watumishi wa Umma Mwanza wakumbushwa kutambua wajibu wao*


Mwenyekiti wa Tume ya Utumishi wa Umma Mhe.Jaji mstaafu Hamissa Kalombola amewataka watumishi wa Umma kufanya kazi huku wakitambua wajibu na stahiki zao ili kuepusha migogoro pale linapokuja suala la kuchukuliana hatua za kinidhamu.

Akifungua leo Mkutano wa kikao kazi kwenye ukumbi wa Rock City Mall kilichowahusisha watumishi wa Umma, Mwenyekiti Mhe.Amisa amesema Tume yake imekuwa ikipokea mashauri mengi yanayochangiwa na watumishi kutofahamu au kuzembea kizingatia miongozo iliyopo ya Utumishi wa Umma.

Ameongeza kuwa Tume yake inachukua hatua ya kutembelea watumishi mikoani lengo likiwa kupeana elimu na kukumbushana kufanya kazi kwa maadili ili kila mmoja atimize majukumu yake na kufikia malengo.

"Maafisa Utumishi mliopo hapa nyie mna wajibu wa kuwafahamu vizuri watumishi wenu na hata anapotokea mtumishi amebadilika ghafla tabia kama utoro,muite msikilize nini tatizo kabla hujamchukulia hatua." Mhe. Hamissa Kalombola

Naye Kamishna wa Tume hiyo, Mhe.Balozi Adadi Rajabu amebainisha Tume yao ina malengo makuu matatu ambayo ni Ushauri kwa Mhe.Rais, ulekevu na kusimamia utoaji wa haki, lengo kwa ujumla watumishi wote wa Umma nchini wafanye kazi katika mazingira sahihi na rafiki.

"Mhe Rais wetu siku zote anapenda kuwaona watumishi wa Umma wakifurahia mazingira yao ya kazi mfano mzuri tumemsikia akizungumza wakati wa Mei Mosi Kitaifa mwaka huu Mkoani Morogoro, hivyo sisi watumishi wajibu wetu ni kurudisha asante kwa kufanya kazi kwa uadilifu ili kulijenga Taifa," Amesema Mhe.Balozi Adadi Rajabu.

Awali alimkaribisha Mwenyekiti wa Tume hiyo,Ndg.Daniel Machunda Katibu Tawala Msaidizi,Utawala na Rasilimali watu akimwakilisha Katibu Tawala wa Mkoa wa Mwanza,amesema kikao kazi hicho kwa watumishi wa Umma kitakuja na matokeo chanya ya uwajibikaji makazini huku kila mmoja akiheshimu Sheria zilizopo.

"Tunajitahidi kufanya kazi kwa kizingatia Sheria,kanuni na taratibu zilizopo na wakati mwingine kukumbushana  miongozo inavyotaka,"Machunda.

Kikao kazi hicho kimewashirikisha watumishi kutoka Ofisi ya Mkuu wa Mkoa,ofisi ya Mkuu wa Wilaya Nyamagana,watumishi wa Jiji la Mwanza na Manispaa ya Ilemela.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.