• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

WAZIRI MKUU AWATAKA WANAMALYA KUCHANGAMKIA FURSA YA CHUO CHA MICHEZO

Posted on: May 18th, 2025

WAZIRI MKUU AWATAKA WANAMALYA KUCHANGAMKIA FURSA YA CHUO CHA MICHEZO


Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Kassim Majaliwa Majaliwa (Mb.) amewataka Wananchi wa eneo la Malya Wilayani Kwimba kujipanga kuboresha na kufanya maendeleo kwa kuwa uwepo wa Chuo cha Michezo katika eneo hilo ni fursa muhimu ya kiuchumi.

Waziri Mkuu ametoa rai hiyo leo mei 18, 2025 alipokuwa katika ukaguzi wa maendeleo ya ujenzi wa Chuo cha Michezo Malya (Sports Academy) ambapo amewataka wananchi kuhakikisha wanajenga miundombinu bora ya malazi na makazi kwa kuwa siku za usoni mji huo unakwenda kubadilika.

“Zaidi ya biliono 32 zitaletwa hapa kuubadili mji huu wa Malya, jipangeni vizuri huu mji unakwenda kubadilika”. Amesisitiza Waziri Mkuu.

Kutakuwa na wageni, wachezaji wa mpira kutoka maeneo mbalimbali watalala wapi? wataishi wapi? watakula wapi?, mna kila sababu ya kujipanga kweli kweli na hii ndio Malya anayoitaka Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan. Ameongeza Mhe. Waziri Mkuu.

Sambamba na hayo Mhe. Waziri Mkuu amepongeza kasi ya mradi hio na ubora wa majengo, na amesema kuwa ameridhishwa kusikia kuwa hakuna deni fedha zinazotakiwa kuletwa zimeletwa kwa wakati.

Katika Taarifa ya Mradi iliyosomwa na Bw. Gerson Msigwa Katibu Mkuu Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo imesema mradi huo ni moja ya miradi ya mkakati ya Serikali ya awamu ya sita ya kuhakikisha inaendeleza selta ya michezo katika Mkoa wa Mwanza na maeneo mengine nchini.

Kwa upande wake Waziri wa Habari, Sanaa, Utamaduni na Michezo Mhe. Professa Palamagamba Kabudi amesema Mradi huo utatekelezwa katika awamu mbili, ambapo awamu ya kwanza itachukua muda wa miezi kumi na mbili (12) na awamu ya pili ni muda wa miezi sita.

Aidha amesema jumla ya kiasi cha shilingi 31,523,920,683.60 kimetengwa na Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia Wizara ya Habari Sanaa Utamaduni na Michezo kwa ajili ya utekelezaji wa mradi huo ambazo zimepangwa kulipwa katika awamu mbili(2).

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • WAZIRI MKUU AWATAKA WANAMALYA KUCHANGAMKIA FURSA YA CHUO CHA MICHEZO

    May 18, 2025
  • NIA YA SERIKALI KILA MWANANCHI AUNGANISHIWE MAJI NYUMBANI KWAKE - WAZIRI MKUU

    May 18, 2025
  • MAKUZI YA AWALI YA MTOTO MSINGI WA UJENZI WA TAIFA IMARA - RAS BALANDYA

    May 16, 2025
  • RC MTANDA AWAKARIBISHA MWANZA WANAFUNZI KUTOKA UGANDA

    May 15, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.