• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

Zingatieni Mafunzo kuepusha Serikali kuchukiwa na kuingia gharama za kisheria: Katibu Mkuu Ikulu

Posted on: January 22nd, 2024

Zingatieni Mafunzo kuepusha Serikali kuchukiwa na kuingia gharama za kisheria: Katibu Mkuu Ikulu


Katibu Mkuu Ofisi ya Rais Ikulu Mululi Mahendeka leo Januari 22, 2024 amefungua mafunzo ya Uzingatiaji Sheria, Kanuni na taratibu za utumishi wa Umma kwa Makatibu Tawala Wasaidizi, utawala na Rasilimali watu kutoka Mikoa ya kanda ya ziwa na kuwataka kuzingatia mafunzo hayo ili kuwepo na tija katika utoaji huduma kwa watumishi na wananchi.

Mahendeka amesema kutokana na kutoelewa kwa miongozo ya sheria imechangia kuwepo na mlolongo wa malalamiko kutoka kwa watumishi na wananchi yanayowafika viongozi wa juu hali ambayo imechangia kuzorotesha utendaji kazi wa Taifa kwa ujumla.

"Ndugu washiriki wa mafunzo haya ambao wengi wenu ni watumishi wenzangu,Ofisi ya Rais imeingia gharama ya kuandaa mafunzo haya kwa siku 5 ikitambua umuhimu wake,mkizingatia ipasavyo sheria,kanuni na taratibu mtaepusha Serikali kuchukiwa na kuingia gharama zinazotokana na mashauri yaliyotokana wahusika mliopewa dhamana ya kusimamia kushindwa kuwajibika kikamilifu,"Katibu mkuu Ikulu.

Amebainisha hakuna sababu ya kuwapa kazi ya kutatua kero wa za wananchi na watumishi viongozi wetu wa juu akiwemo Rais,Makamu wa Rais,Waziri Mkuu au Katibu mkuu kiongozi wakati waliopewa jukumu hilo wapo lakini wameshindwa kutimiza wajibu wao.

"Kushindwa kutafsiri vizuri sheria,kanuni na taratibu imechangia watumishi kutumia muda mwingi kwenye vyombo vya kisheria kusaka haki yao na kushinda mashauri yao na mwishowe Serikali kuingia gharama," Xaveri Daud Naibu Katibu mkuu OR-Menejimenti ya utumishi wa umma

Mwenyeji wa mafunzo hayo ambaye ni Katibu Tawala mkoa wa Mwanza Ndg.Balandya Elikana ameishukuru Ofisi ya Rais kwa kuyaleta mafunzo hayo Mkoani humo na kuwataka washiriki wote kuja na matokeo chanya baada ya kuelimishwa vyema.

"Tunapotoa huduma bora kwa wananchi na watumishi Imani kutoka kwao inazidi kuongezeka kwa Serikali hali itakayo kuwa na tija katika utendaji kazi kwa ujumla," Katibu Tawala mkoa.

Washiriki wengine katika mafunzo hayo wanatoka kwenye Taasisi za Serikali wataalamu wa sheria na Rasilimali watu kutoka mikoa ya Shinyanga,Mara,Geita,Simiyu,Mara,Kagera na Mwanza.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.